Serikali Yawarejesha Kazini Watumishi wa Darasa la Saba Waliokuwa Kazini Kabla ya Mei 20, 2004.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.
Serikali imeamuru kurudishwa kazini kwa Watumishi wote ambao walikuwa na ajira za kudumu au ajira za mikataba (kwa watendaji wa Vijiji na Mitaa) au ajira za muda ambao walikuwa kazini kabla ya Mei 20, 2004 ulipoanza kutumika waraka wa Utumishi Na. 1 wa mwaka 2004 ambao umetaja kuwa cheti cha ufaulu wa mtihanai wa kidato cha nne kama sifa ya msingi kwa mtumishi wa Umma.

Kauli hiyo imetolewa leo bungeni Mjini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika alipokuwa akitoa Kauli ya serikali kuhusu watumishi waliondolewa kwenye mfumo wa malipo ya mshahara kwa kukosa sifa ya cheti cha kufaulu mtihani wa elimu ya kidato cha nne.

"Watumishi wa Umma Elfu Moja Mia Tatu Sabini (1,370) waliolegezewa masharti ya sifa za muundo kupitia barua ya Katibu Mkuu Utumishi yenye Kumb. Na. CCB.271/431/01/p/13 ya tarehe 30 Juni, 2011 warejeshwe kazini mara moja, walipwe mishahara yao kwa kipindi chote ambacho walikuwa wameondolewa kazini na waendelee na ajira zao hadi watakapostaafu kwa mujibu wa Sheria," alisema Mhe. Mkuchika.

Hata hivyo amesema kuwa uamuzi huu uliotajwa hautawahusu watumishi wawasilisha vyeti vya kughushi katika kumbukumbu za ajira zao, watumishi waliokuwepo katika ajira kabla ya tarehe 20 Mei, 2004 pamoja na warumishi wote walioajiriwa baada ya tarehe 20 Mei 2004 wakiwa hawana sifa za kufaulu mtihani wa kidato cha nne kwa kuwa walijipatia ajira kinyume cha maelekezo ya Serikali.

Aidha, watendaji wakuu wa Idara za Utawala na Utumishi wote walioshiriki kuwaajiri Watumishi wasiokuwa na sifa ya kufaulu mtihani wa kidato cha nne katika Utumishi wa Umma baada ya tarehe 20 Mei, 2004 watachukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa sheria, kanuni za taratibu.

Vilevile watendaji wakuu na maafisa wote wanaosimamia zoezi hili ambao kwa namna yoyote ile watashiriki kuhujumu zoezi hili kwa kuondoa au kuharibu kumbukumbu za Watumishi ili haki isitendeke, watachukuliwa hatua za kinidhamu na za kijinai ikibidi.


MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI LEO APRIL 9, 2018

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harisson Mwakyembe akiteta jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (kulia) na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza wakati wa Mkutano wa Bunge la Kumi na Moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, elo Mjini Dodoma.
Naibu Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Mhandisi Stella Manyanya akijibu maswali ya wabunge, wakati wa Mkutano wa Bunge la Kumi na Moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo Mjini Dodoma.
Naibu Waziri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Ole Nasha akijibu hoja za wabunge, wakati wa Mkutano wa Bunge la Kumi na Moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo Mjini Dodoma.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimweleza jambo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, wakati wa Mkutano wa Bunge la Kumi na Moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongoza Mkutano wa Bunge la Kumi na Moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo Mjini Dodoma.

 

NAIBU SPIKA TULIA AWAASA WATANZANIA KUILINDA NA KUITUNZA AMANI YA NCHI TAMASHA LA PASAKA MJINI DODOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu Spika wa Bunge Mh. Dk. Tulia Ackson akikata utepe kuashiria uzinduzi wa albamu mpya ya Mwimbaji mahiri wa nyimbo za Injili. Rose Muhando ijulikanayo kwa jina la 'Usife Moyo'wakati wa kilele cha tamasha la pasaka katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma jana jioni.Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo Dkt. Mary Mwanjelwa na kushoto  ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion na mwandaaji wa tamasha hilo Alex Msama.
Naibu Spika wa Bunge Mh. Dk. Tulia Ackson kwa pamoja na viongozi wengine wakifurahia jambo mara baada ya uzinduzi wa albamu mpya ya Rose Muhando ijulikanayo kwa jina la  'Usife Moyo',.
Mgeni rasmi katika tamasha la pasaka 2018,Naibu Spika wa Bunge Mh. Dk. Tulia Ackson akizungumza mbele ya umati wa watu (hawapo pichani),waliofika kushuhudia waimbaji wa nyimbo za injili wakitumbuiza katika tamasha hilo mapema jana katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.Dkt Tulia aliwaasa Watanzania kuilinda  na kuitunza amani ya nchi kwa gharama yoyote,kwani wakiichezea amani waliyonayo kuipata tena haitakuwa rahisi,hivyo akaongeza kwa kuwaomba Watanzania waishi kwa upendo,kushirikiana kwa namna moja ama nyinine na pia kushiriki katika suala zima la kujenga uchumi wa nchi yao na hatimae kupiga hatua katia suala zima la maendeleo.
Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira ambaye pia ni Mbunge wa Dodoma mjini,Mh.Anthony Mavunde akitoa neno la shukurani kwa kampuni ya Msama Promotions Ltd kwa kuandaa tamasha la pasaka 2018 mjini humo na kuwakusanya Wakazi wa mji wa Dodoma na vitongoji vyake,kuja kujionea waimbaji mahiri wa nyimbo za injili ndani ya uwanja wa Jamhuri.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions Ltd,Alex Msama ambaye ndiye Muaandaji wa tamasha la pasaka 2018 akiwashukuru wakazi wa Dodoma na Vitongoji vyake waliojitokeza kwa wingi katika tamasha la pasaka ndani ya uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.Kushoto ni Naibu Spika wa Bunge Mh. Dk. Tulia Ackson,Naibu Waziri wa Kilimo Dk. Mary Mwajelwa pamoja na Rose Muhando.
Naibu Spika wa Bunge Mh. Dk. Tulia Ackson akicheza na Mwimbaji Rose Muhando, Mwimbaji Bonny Mwaiteje na Naibu Waziri wa Kilimo Dk. Mary Mwajelwa na baadhi ya wabunge mara baada ya kuzindua albam yake inayoitwa “Usife Moyo” kwenye tamasha la pasaka lililofanyika ndani ya uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma jana jioni.Kulia ni Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion na mwandaaji wa tamasha hilo Bw. Alex Msama.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Utawala Bora Mh. Kapteni George Mkuchika akizungumza katika tamasha hilo huku Naibu Spika Dk.Tulia Ackson na baadhi ya viongozi wengine wakimsikiliza.
Sehemu ya Meza kuu,ikifurahi yaliyokuwa yakijiri uwanjani huku waimbaji wakiendelea kuimba kwa zamu ndani ya tamasha la Pasaka jana jioni mjini Dodoma.
Sehemu ya Meza kuu ilipoamua kushuka na kwenda jukwaani kuunga mkono na kutoa neno la shukurani kufuatia kufanyika tamasha la Pasaka jana jioni mjini Dodoma.


KITUO CHA DALADALA JAMATINI KUENDELEA KUTUMIKA, MABASI YA MIKOANI YAONYWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi akifafanua jambo wakati Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge alipozungumza na wadau wa usafishaji katika Stendi Kuu ya muda ya Mabasi ya Mikoani iliyopo eneo la Nanenane jana Aprili 3, 2018 alipofanya ziara fupi katika stendi hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge akizungumza na wadau wa usafishaji katika Stendi Kuu ya muda Mabasi ya Mikoani iliyopo eneo la Nanenane jana Aprili 3, 2018 alipofanya ziara fupi katika stendi hiyo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (katikati) akifafanua jambo wakati Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge (kushoto) alipofanya ziara fupi kukagua maeneo yanayoweza kuwekewa miundombinu muhimu na kutumika kama kituo cha daladala cha Mjini, jana Aprili 3, 2018. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Ujenzi Mhandisi Ludigija Ndwata. 


Na Ramadhani Juma,Ofisi ya Mkurugenzi

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge ameelekeza matumizi ya kilichokuwa kituo Kikuu cha Mabasi madogo maarufu kama Daladala cha Jamatini Mjini Dodoma kwa ajili ya kupakia na kushusha abiria wanaotoka katika maeneo mbalimbali ya Manispaa hiyo yaendelee kama kawaida wakati Manispaa ikiandaa eneo mbadala.

Mkuu huyo wa Mkoa pia ameagiza ‘ruti’ za Daladala zifupishwe kama ilivyokuwa awali, na kwamba upangaji wa ‘ruti’ ndefu ujadiliwe upya na wadau wote wanaohusika na endapo utakubaliwa na wengi ndipo utekelezaji wake uanze.

Dokta Mahenge ametoa maelekezo hayo leo Aprili 3, 2018, alipokuwa akizungumza na wadau wa usafirishaji katika kituo kikuu cha mabasi ya Mikoani cha muda kilichopo Nanenane Manispaa ya Dodoma baada ya kituo hicho kufungwa wiki iliyopita kwa ajili ya kupisha mradi wa Reli ya Kisasa.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya majadiliano na wadau wote ikiwemo Mamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMTRA), Manispaa, Jeshi la Polisi, na Shirika la Reli ambao ndio wamiliki wa eneo hilo, na kwamba matumizi ya stendi hiyo yataendelea kwa muda wa miezi miwili kuanzia sasa, kipindi ambacho Manispaa itatakiwa kuwa imeshapata na kuandaa stendi mbadala.

Akizungumza katika eneo la tukio, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi alisema Manispaa imepokea maagizo yote na itahakikisha inaandaa eneo kwa ajili ya Stendi ya Mabasi madogo Mjini katika kipindi cha miezi miwili kama ilivyoelekezwa na Mkuu wa Mkoa.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa ameagiza mabasi yote yanayosafirisha abiria Mikoa mbalimbali Nchini kupakia na kuanzia safari zao katika kituo Kikuu cha mabasi ya muda kilichopo Nanenane na Kampuni itakayokiuka itachukuliwa hatua kali za Kisheria.

“Namuagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani wa Mkoa kuwa, kuanzia kesho mabasi yote yauze tiketi na kuanza safari zao hapa katika kituo hiki Kikuu cha mabasi cha muda cha Nanenane…hakuna Mkubwa wala mdogo katika kutoa huduma kwa Wananchi” alisisitiza Dkt. Mahenge.

UKARABATI WAANZA KULETA NURU KONDOA GIRLS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

KAMATI YA BUNGE YA BAJETI YAENDELEA NA VIKAO VYAKE MJINI DODOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Hawa Ghasia akizungumza na Wajumbe wa kamati hiyo pamoja na viongozi wakuu kutoka Wizara ya fedha na Mipango walioongozwa na Waziri wa fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango wakati wa kupitia na kujadili Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa fedha 2018/2019, katika kikao kilichofanyika leo ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.
Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Albert Ntabaliba akizungumza wakati wa kupitia na kujadili Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa fedha 2018/2019 katika kikao kilichofanyika leo ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.

  Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Hawa Ghasia akizungumza na Wajumbe wa kamati hiyo pamoja na viongozi wakuu kutoka Wizara ya fedha na Mipango (hawapo kwenye picha) wakati wa kupitia na kujadili Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa fedha 2018/2019. Kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango katika kikao kilichofanyika leo ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.
Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Maria kangoye akizungumza wakati wa kupitia na kujadili Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa fedha 2018/2019 katika kikao kilichofanyika leo ukumbi wa Pius Msekwa Mjini Dodoma. kushoto ni Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Riziki Lulidi
(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

MWANZO HABARI KITAIFA HABARI KIMATAIFA BURUDANI TANGAZA HAPA WASILIANA NASI Uncategories UVCCM WAAPA KUPAMBANA NA YEYOTE ANAYEICHAFUA NCHI UVCCM WAAPA KUPAMBANA NA YEYOTE ANAYEICHAFUA NCHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Taifa UVCCM, Kheri James amewataka vijana wa umoja huo kuwa tayari kulinda heshima ya nchi kwa gharama yeyote dhidi ya vibaraka ambao wanataka kuchafua taswira ya nchi kwa lengo la kuwanufaisha mabeberu.

Kheri ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na vijana wa umoja huo mjini Dodoma na kusema lengo la kufanya hivyo ni kutokana na kuwepo na matumaini makubwa ya kiuchumi yaliyorejeshwa na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli hivyo hawapo tayari kuona kikundi cha watu wachache wanaotaka kuwarudisha nyuma kimaendeleo.

"Kuanzia sasa endapo akiibuka mtu mwenye ujasiri wa kutukana, vijana hawatotukana bali watafanya litakaloonekana linafaa kwa maslahi ya taifa kwani wapo wanaojipambanua wazi kusifu viongozi wa ulimwengu mzima lakini kamwe hawawezi kuwapongeza na kuwasifu kwa chochote viongozi wa nchi", amesema Kheri James.

Naye Kaimu Katibu UVCCM, Shaka Hamdu Shaka amesema serikali imeona uwepo wa vijana makao makuu na kuthamani uwepo wao kutokana na kuendesha mambo kisasa zaidi.

Kwa upande wake mbunge wa viti maalum vijana, Mariam Mzuzuri amesema maamuzi na tamko la mwenyekiti wa uvccm taifa watalifanyia kazi ili vijana waweze kutambua fursa walizonazo hususania mkoani Dodoma ambako hivi sasa ni makao makuu ya nchi

KATIBU MKUU OFISI YA WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi (katikati) akisisitiza jambo wakati akifungua Kikao cha Baraza la wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu lililofanyika tarehe 21Machi, 2018 mjini Dodoma.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akiimba wimbo wa Umoja na Mshikamano pamoja na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Ofisi hiyo leo mjini Dodoma kabla ya kufungua Kikao hicho.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakiimba wimbo wa Umoja na Mshikamano leo mjini Dodoma kabla ya kufunguliwa kwa Kikao cha baraza hilo .

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Bunge na Waziri Mkuu Bi. Maimuna Tarishi ameongoza Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo na kuwaasa wajumbe wa baraza kutoa maoni yatakayosaidia kufanikisha mchakato wa maandalizi ya Bajeti ya mwaka 2018/2019.

Akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao hicho Tarishi amesema kuwa Watumishi wote katika Ofisi hiyo wanao wajibu wakushiriki kikamilifu katika mchakato wa maandalizi ya bajeti ili kufanikisha azma ya Serikali kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

“Bila kujali nafasi zenu ni lazima mtambue kuwa mnao wajibu sawa katika kutoa maoni yatakayosaidia katika mchakato wa maandalizi ya bajeti” alisisitiza Bi. Tarishi.

ATUMIA MIEZI SABA KUSAFIRI KWA PIKIPIKI KUTOKA OMAN HADI TANZANIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akiteta jambo na Maher Al Barwani kutoka nchi ya Oman mwenye asili ya Tanzania ambaye amesafiri kwa muda wa miezi saba kupitia mataifa mbalimbali hadi kufika Tanzania kwa pikipiki kwa lengo la kuimarisha uhusiano uliopo baina ya nchi hizo mbili pamoja na kutangaza utalii wa Tanzania nchini humo, alipotembelea ofisi za Wizara hiyo mjini Dodoma. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akiteta jambo na Maher Al Barwani kutoka Oman mwenye asili ya Tanzania ambaye amesafiri kwa muda wa miezi saba kupitia mataifa mbalimbali hadi kufika Tanzania kwa pikipiki kwa lengo la kuimarisha uhusiano uliopo baina ya nchi hizo mbili pamoja na kutangaza utalii wa Tanzania nchini humo alipotembelea ofisi za Wizara hiyo mjini Dodoma jana. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Aloyce Nzuki na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala, Tutubi Mangazeni. 
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Aloyce Nzuki akiteta jambo na Maher Al Barwani kutoka Oman mwenye asili ya Tanzania ambaye amesafiri kwa muda wa miezi saba kupitia mataifa mbalimbali hadi kufika Tanzania kwa pikipiki kwa lengo la kuimarisha uhusiano uliopo baina ya nchi hizo mbili pamoja na kutangaza utalii wa Tanzania nchini humo alipotembelea ofisi za Wizara hiyo mjini Dodoma jana. Kulia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga
 Picha ya pamoja ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) na Maher Al Barwani, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dk. Aloyce Nzuki na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala, Tutubi Mangazeni.
 Maher al Barwani akimuelezea Ndugu David ambeye ni Afisa Usafirishaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii jinsi alivyoweza kutumia usafiri huo wa pikipiki kutoka nchini Oman hadi Tanzania.
 Maher al Barwani anapatikana kupitia Mawasiliano hayo.
 Kwa muda wa miezi saba Maher al Barwani ameweza kusafiri umbali wa kilomita 18,035.6 kutoka Oman hadi ofisi za Makao Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma.
 Pikipiki anayotumia aina ya BMW ina uwezo wa kukimbia kwa spidi 240.
Maher al Barwani akiondoka baada ya kusalimiana na viongozi wa viwaza mjini Dodoma. (PICHA NA HAMZA TEMBA-WMU-DODOMA)
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa