Home » » JK ATAKIWA KUNUSURU MCHAKATO KATIBA MPYA

JK ATAKIWA KUNUSURU MCHAKATO KATIBA MPYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MCHUNGAJI wa Kanisa la PAG, Charles Kanyika, amemtaka Rais Jakaya Kikwete, kushirikiana na viongozi wastaafu kunusuru nchi katika kipindi hiki cha kuelekea kutunga Katiba mpya.
Mchungaji Kanyika alisema Rais Kikwete alianza kuiweka nchi katika hatua mbaya baada ya kutoa hotuba ya kufungua Bunge Maalumu, iliyokuwa na lengo la kutetea msimamo wa chama anachotoka.
 “Tunakoelekea hawa viongozi wa siasa watatuingiza mahali pabaya wamekuwa wakitoa matamko ambayo yanawachanganya wananchi na kuhusu huu mchakato kuna kila sababu akawahusisha viongozi ambao ni maarufu ili wakae meza moja ili kutafuta mwafaka.
“Jambo la msingi na la muhimu ni kuwaomba marais wastaafu pande zote mbili mawaziri wakuu pande zote mbili na majaji na wanasheria pande zote mbili kukaa meza moja na ili kufanikiwa mwenyekiti wa kikao hicho awe rais wa Pili Ali Hassan Mwinyi,” alitoa ushauri huo Mchungaji Kanyika.
 Alisema anawapongeza wajumbe wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kwa kususia mijadala ya Bunge kwa kuwa kilichokuwa kikijadiliwa ni msimamo wa CCM badala ya rasimu iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
 “Kinachotakiwa kujadiliwa si serikali mbili, wajumbe wanatakiwa kujadili kile kilichopo katika rasimu ya Katiba ambayo ni serikali tatu, hayo si mawazo ya tume bali ni mawazo ya wananchi,” alisema. 
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa