Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Dodoma. Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika na Mbunge wa
Kasulu(NCCR-Mageuzi), Moses Machali, kwa nyakati tofauti wamesema
mjadala unaoendelea bungeni bila kuwepo kundi la Ukawa, haliwezi kutoa
Katiba Mpya.
Akizungumza juzi, Mnyika alisema Katiba lazima
ipatikane kwa maridhiano hivyo busara ingetumika kutafuta utaratibu
mwingine wa kuendelea na Bunge Maalumu badala ya kulazimisha mambo.
Alisema wamesusia Bunge hilo kwa sababu za msingi,
moja kati ya sababu hizo anaitaja kuwa ni kulazimishwa kujadili masuala
ya Serikali mbili, ilhali ni tofauti na mfumo unaopendekezwa kwenye
rasimu ambayo ndiyo mwongozo wa mijadala hiyo.
Mnyika alisema wanaoendelea kujadili rasimu hiyo
kwa lengo la kupata Katiba Mpya, wanapoteza muda na rasilimali kwa kuwa
lazima kuwe na maridhiano ya pande mbili.
Naye Moses Machali alisema hawakukosea kususia
Bunge hilo kwa kuwa lengo lao la kufikisha ujumbe limetimia. Pia hiyo ni
sehemu ya kutekeleza malengo maalumu waliyojiwekea.
Machali aliongeza kusema kuwa Rasimu ya Katiba
yenye muundo wa Serikali mbili inakihusu zaidi chama tawala (CCM), ndiyo
maana wamekiachia chama hicho na washirika wake waendelee nayo.
“Tumejiridhisha, badala ya kujadili rasimu sura
kwa sura, walilazimisha ianzwe sura ya kwanza na sita zinazohusu muundo
ili wafumue muundo na kuweka wa Serikali mbili. Waendelee na Katiba yao
ya CCM sisi hatuhusiki nayo,” alieleza Machali ambaye mara nyingi
michango yake bungeni huonekana kuwa mwiba.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment