Home » » MNYIKA;SIJA ONDOSHA HOJA YA KUIKATAA HATI YA MUUNGANO

MNYIKA;SIJA ONDOSHA HOJA YA KUIKATAA HATI YA MUUNGANO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mjumbe wa Bunge la Katiba, John Mnyika amesema hajaondoa hoja yake ya kutaka kuwekwa wazi mkataba halisi wa Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.
Akizungumza na gazeti hili, Mnyika alisema hoja hiyo haijafa licha ya mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta kusema imepelekwa katika kamati na sasa ni zaidi ya wiki mbili haijatolewa maelezo.
Mnyika, ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Ubungo kwa tiketi ya Chadema, alisema anakusudia kuirudisha hoja hiyo bungeni.
“Natarajia tukianza majadiliano katika sura hizi mbili, sura ya kwanza na ya sita, niombe tena hati halisi kwani ndio msingi wa majadiliano hasa kuhusiana na mambo ya Muungano,” alisema .
Alisema kuirejesha hoja hiyo itakuwa ni utekelezaji wa kanuni za Bunge la Katiba, kwani bado haijapatiwa majibu lakini ni hoja yenye msingi mkubwa hasa katika majadiliano ya Bunge hilo.
Mnyika aliwasilisha hoja ya kuomba kupatiwa hati halisi ya Muungano wakati bunge hilo lilipoanza, lakini hata hivyo, hadi sasa haijapatiwa ufumbuzi. Hadi sasa wajumbe wa  Bunge hilo wamepewa nyaraka zenye maudhui ya hati hiyo.
“Ni ukweli tumepewa Sheria ya Tangayika kuridhia Muungano Sheria Namba 22 ya mwaka 1964, lakini sheria hii ina maudhui tu ya Muungano siyo hati ambayo mimi naihitaji,” alisema Mnyika.
Tangu kuanza vikao vya kamati za Bunge hilo, hoja ya kutakiwa Hati ya Muungano ilijitokeza katika kamati zote 12.
Jambo hilo liliulazimisha uongozi wa  Bunge kumwita Dodoma aliyekuwa katibu wa Bunge la Tanganyika, Pius Msekwa kutoa ufafanuzi kuhusu hati na sheria ya kuridhia Muungano.
Hata hivyo, ufafanuzi wa Msekwa unaonyesha haukuwakuna wajumbe wengi wa Bunge hilo.
chanzo:mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa