Home » » NCHEMBA,POLEPOLE WATOFAUTIANA KUHUSU GHARAMA ZA SHIRIKISHO

NCHEMBA,POLEPOLE WATOFAUTIANA KUHUSU GHARAMA ZA SHIRIKISHO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesema vyanzo vya mapato vilivyopendekezwa katika Rasimu ya Katiba, havitoshi kuendesha Serikali ya shirikisho.
Nchemba aliyasema hayo katika kipindi cha Tuongee, kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Star TV kila asubuhi.
“Sijui kama ilikuwa ni makusudi Serikali ya shirikisho itengenezwe halafu iishie njiani, kwanza tafsiri ya ushuru wa bidhaa ni finyu,” alisema. Kwa mujibu wa Mwigulu tafsiri ya ushuru wa bidhaa inajumuisha forodha, ushuru wa bidhaa, kodi ya mauzo, kodi ya ongezeko la thamani (VAT), kodi ya mazao na kodi ya mauzo ya nje.
Alisema kwa tafsiri hiyo pana, makadirio yake yanaweza kwenda hadi Sh4 trilioni na kuendelea.
Hata hivyo, aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphery Polepole alisema waliziita taasisi zote za fedha na kupata nafasi ya kujua makusanyo, matumizi na jinsi matumizi ya muungano yanavyokuwa.
Polepole alisema kulingana na uchambuzi walioufanya, fedha inayotakiwa kuendesha Serikali ya shirikisho ipo na kwamba mapato hayo yanatosha kuendesha Serikali hiyo.
Alisema imethibitika matumizi makubwa ya fedha yanatumika Tanzania Bara kuliko Zanzibar na gharama za Muungano ambazo ni Sh1.8 trilioni ni ndogo ikilinganishwa na zile za pande zote mbili za Muungano.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa