Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kwa upande wake Zitto, naye alimpongeza CAG kwa kukagua vyama vya siasa akisema ni kati ya maeneo yaliyokuwa na matatizo
Ukaguzi uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali
(CAG), katika vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu umebaini madudu
ikiwamo vyama vinne kutokuwa na akaunti benki.
Akizungumza na waandishi wa habari bungeni mjini
Dodoma jana, CAG Ludovick Utouh alivitaja vyama ambavyo havina akaunti
benki kuwa ni UMD, NLD, NRA na ADC.
“Katika hesabu walizotuletea kulikuwa hakuna
ushahidi kwamba wanaendesha akaunti benki,” alisema huku akibainisha
kuwa kitendo hicho ni kinyume na Kifungu cha 15(1) cha Sheria ya Vyama
vya Siasa.
Halikadhalika katika ukaguzi huo, vyama vya siasa
11 kati ya 21 vyenye usajili wa kudumu, havikuwasilisha taarifa za
hesabu za mwaka kama Kifungu cha 14(1) cha sheria hiyo ya mwaka 1992
kinavyosema.
Alipoulizwa baadaye vyama hivyo, Utouh alivitaja
CCK, UPDP, Tadea, Demokrasia Makini, Chausta, DP na AFP. Vyama vya Sauti
ya Umma na Chauma viliwasilisha hesabu zao vikiwa vimechelewa.
Utouh alisema katika ukaguzi huo, taarifa za
hesabu zilizowasilishwa na vyama 10 hazikufuata misingi ya mfumo wa
utoaji wa taarifa za fedha za kimataifa.
“Tulibaini kuwa hakuna chama cha siasa hadi sasa
kilichowasilisha kwa msajili wa vyama vya siasa tamko la mali zote
zinazomilikiwa na chama husika jambo ambalo ni kinyume cha sheria,”
alisema.
Utouh alitumia mkutano wake huo na wanahabari
kumpongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC),
Kabwe Zitto kwa kusimama kidete ku
hakikisha vyama vya siasa navyo vinakaguliwa na CAG kama sheria inavyoelekeza.
hakikisha vyama vya siasa navyo vinakaguliwa na CAG kama sheria inavyoelekeza.
Kwa upande wake Zitto, naye alimpongeza CAG kwa kukagua vyama vya siasa akisema ni kati ya maeneo yaliyokuwa na matatizo.
“Kwa kitendo chako cha kuamua kukagua bila hata ya
kupewa fedha ni kitendo ambacho kinaonyesha uzalendo wako wa hali ya
juu,” alisema Zitto na kuongeza:
“Kwa sababu tunachokitaka sisi ni kila senti ya
mlipa kodi ikaguliwe na kama nilivyowahi kusema huko nyuma kwa miaka
minne vilikuwa vimepewa ruzuku ya Sh69 bilioni.”
Zitto alihoji kama CAG anakwenda kukagua bodi za
mazao nchini ni kwa nini vyama vya siasa visikaguliwe wakati ndivyo
vinavyozalisha Serikali pale vinaposhinda uchaguzi?
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment