Home » » HALMASHAURI ZOTE SASA KUBANWA

HALMASHAURI ZOTE SASA KUBANWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Halmashauri zote nchini zimetakiwa kutenga bajeti ya mwaka huu ya asilimia 60 ya makusanyo yake ya ndani kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi.
Akiwasilisha maoni ya Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bungeni jana kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Tamisemi, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Hamis Kigwangala alisema kamati yake haitakubaliana na bajeti ya halmashauri yoyote ile kama haijakidhi matakwa ya agizo hilo na kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi) imepewa kazi kuhakikisha agizo hili la kamati linatekelezeka.
Dk Kigwangala alisema kamati inaendelea kuzisisitiza sekretarieti za mikoa zikiongozwa na wakuu wa mikoa, kuimarisha ufuatiliaji na kuzisimamia halmashauri na kuhakikisha kuwa, fedha za miradi ya maendeleo zitokanazo na makusanyo ya ndani na nje zinatumika kuwaletea wananchi maendeleo.
Alisema kamati yake pia imependekeza Serikali kuweka mikakati madhubuti ya ukusanyaji wa mapato ya majengo katika miji, manispaa, na miji midogo, kwani fedha nyingi zinapotea kwa kutokusanywa kwa kodi hii.
Alisema kuwa Kamati inatambua kuwa agizo hili limeshaanza kutekelezwa na Serikali, hata hivyo kwa yale maeneo ambayo yameainishwa kutakiwa kufanyiwa tathimini kuhusu thamani halisi ya majengo hayo kwa ajili ya kutozwa kodi ya majengo.
Alizitaka halmashauri kutumia mapato yake ya ndani kukamilisha miradi ya ujenzi wa majengo ya madarasa, majengo ya zahanati na vituo vya afya, nyumba za walimu, nyumba za wauguzi vijijini, mabarabara ya vijijini, kuchimba visima.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa