Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),
amezinyooshea kidole mamlaka mbili za Serikali kwa kushindwa kudhibiti
uingizaji wa bidhaa zisizo na ubora nchini.
Taarifa ya CAG kuhusu ukaguzi wa ufanisi na
ukaguzi maalumu kwa kipindi kinachoishia Machi 31, 2014, imezitaja
taasisi hizo kuwa ni Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Mamlaka ya
Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), akisema zilipwaya katika ukaguzi wa
ubora wa chakula kinachoingizwa na kuzalishwa nchini.
Taarifa hiyo imebainisha kuwa ufuatiliaji ulishindwa kuzuia viwanda vya usindikaji chakula kuvunja sheria mara kwa mara.
Kwa mujibu wa CAG, asilimia 80 ya viwanda
vilivyokuwa vimekiuka sheria havikuchukuliwa hatua, huku kukiwapo makosa
ya kujirudiarudia kwa wasindikaji na waagizaji chakula nje ya nchi.
Taarifa hiyo imesema kwa hali inavyoonekana, idadi
ya bidhaa hafifu nchini imekuwa ikiongezeka kwa miaka mitatu kwa kati
ya asilimia 30 na 40 kutoka mwaka wa fedha wa 2010/2011.
Bidhaa hizo nyingi hupita katika bandari na mipaka
ya Tanzania ambayo wakaguzi wa TBS walitakiwa kuzikagua, lakini
kutokana na upungufu wa ukaguzi, zimekuwa zikiingia nchini.
Katika taarifa hiyo, CAG alisema ukaguzi wa ubora
wa bidhaa zinazoingia nchini haukufanyika vizuri na vya kutosha na
ukaguzi wa bidhaa kutoka nje haukufanywa kwa kuzingatia viashiria
hatarishi.
“Bidhaa zote zilipewa kipaumbele sawa wakati wa
ukaguzi licha ya ukweli kwamba baadhi ya bidhaa zinajulikana kuwa na
athari kubwa kwa afya na mazingira ya walaji nchini,” imesema taarifa
hiyo.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment