Home » » BUNGE LA HOJI WIZARA YA MAJI KUTOPEWA BILIONI 173.8/-

BUNGE LA HOJI WIZARA YA MAJI KUTOPEWA BILIONI 173.8/-

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Profesa Peter Msolla.
Bunge limeeleza kusikitishwa na hatua ya serikali kushindwa  kuipa Wizara ya Maji nyongeza ya Sh. bilioni 173.8 ambazo ni za  miradi ya maendeleo zilizopitishwa mwaka jana ili kuiwezesha wizara hiyo kutekeleza majukumu iliyokuwa imejipangia.
Aidha, Bunge halikuridhishwa na nyongeza kidogo ya Sh. bilioni 46.5  iliyotolewa kati ya jumla kuu iliyoidhinishwa na Bunge jambo lililoifanya wizara hiyo nyeti kuwa na  upungufu wa Sh. bilioni 127. 2  na kushindwa kukamilisha miradi mingi ya maendeleo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Profesa Peter Msolla, alisema pengo hilo limesababisha wizara hiyo kukwama  kutekeleza karibu miradi yote kwa vile  kati ya miradi 1,473 iliyokuwa itekelezwe iliyokamilika ni  228 .

“Bila fedha hizi kutolewa hakuna muujiza  utakaoiwezesha wizara kufikia  malengo  ya kuwafikishia wananchi maji  hasa wa vijijini ambako tatizo ni kubwa  zaidi.”

Profesa Msolla alisema Bunge linaitaka serikali kutoa fedha hizo kama zilivyoidhinishwa ili Wizara itekeleze malengo iliyokusudia.

Mwaka huu wa fedha serikali ilikuwa imeipangia wizara hiyo bajeti ya Sh. bilioni 138 kwa ajili ya miradi ya maji, lakini Bunge liliongeza  Sh. bilioni 184.4 na kuifanya ifikie Sh. bilioni 312.1.

Pia, kamati aliihoji serikali kuhusu kutokamilika kwa miradi mikubwa ya maji ambayo imechukua muda mrefu kama ile ya Kimbiji , Mpera pamoja ujenzi wa bwawa la Kidunda,  upanuzi wa vyanzo vya maji vya Ruvu Juu na Chini.
 
SOURCE: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa