Home » » MIKUTANO YA HADHARA HAIJARUHUSIWA

MIKUTANO YA HADHARA HAIJARUHUSIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Serikali imeendeleza kigugumizi cha kutoruhusu mikutano ya hadhara katika mikoa ya Lindi na Mtwara hadi hapo itakapotangazwa.
Kauli hiyo ilitolewa jana bungeni na Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipokuwa akijibu swali la Seleman Bungala (Lindi Vijijini-CUF).
Mbunge huyo alitaka kauli ya Serikali kuhusu kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na taasisi za kidini katika mikoa ya Lindi na Mtwara kama bado zuio hilo lipo na ni sababu zipi zilisababisha kutolewa kwa amri hiyo.
Bungara (Bwege) alisema hivi sasa kumekuwa na utulivu wa kutosha katika mikoa hiyo jambo linasababisha wananchi kuhoji juu ya viongozi hao kutofanya mikutano.
 Waziri Mkuu alikiri Serikali kuzuia mikutano katika mikoa hiyo kutokana na ukaribu wake na hasa yaliyotokea Mtwara wakati wa vurugu za gesi.
Alisema bado anafuatilia kupitia vyombo mbalimbali na kuona hali haijatulia bado, lakini ukifika wakati akijiridhisha, ataruhusu mikutano hiyo kuendelea.
“Unajua hivi karibuni nilitaka kuruhusu mikutano ya Lindi iendelee kufanyika lakini kuna mambo fulani hayaja kaa sawa,” alisema Pinda.
Alisema ataendelea kufuatilia kupitia vyombo mbalimbali pamoja na wakuu wa mikoa hiyo na akijiridhisha ataruhusu kwa kuwa hata yeye na chama chake wanahitaji kuzungumza na wananchi kwa kuwa uchaguzi mkuu wa mwakani hauko mbali.
Wakati huohuo, Pinda ametangaza kuwa hakuna mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) atakayeshindwa kufanya mitihani yake ya mwisho kwa sababu ya kukosa ada.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa