Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Kebwe Stephen Kebwe
amewataka wananchi kujenga utamaduni wa kupima afya zao ili kuzuia kasi
ya ugonjwa wa Selimundu (Sickle Cell).
Alisema ugonjwa huo unapaswa kupigwa vita kwa
nguvu kwani asilimia 13 hadi 18 ya Watanzania, wanaugua ugonjwa huo
ulioenea kwenye mikoa ya Kanda ya Kati, Kanda ya Ziwa na Pwani.
Dk Kebwe ameiagiza wizara yake kutenga fedha kwa
ajili ya mapambano dhidi ugonjwa huo na kusema kuwa bila jitihada za
makusudi, taifa litazidi kupoteza nguvukazi kutokana na ugonjwa huo.
Aliyasema hayo jana wakati akizundua kampeni ya
kuhamasisha mapambano dhidi ugonjwa huo iliyofanyika kwenye Viwanja vya
Nyerere Squire mjini Dodoma.
“Takwimu zilizotolewa na Shirika la Afya Duniani
(WHO), Tanzania ni nchi ya tano duniani kwa kuwa na wagonjwa wengi wa
ugonjwa huu wa ‘Sickle Cell’”, alisema Dk Kebwe
Alisema kuwa kutokana na ugonjwa huo kuwa tishio
amezitaka pia hospitali zote nchini kufungua kliniki maalumu kwa ajili
ya kupima ugonjwa huo, kwani hivi sasa ni Hospitali ya Taifa Muhimbili
pekee ndiyo inayotoa matibabu ya ugonjwa huo.
“Kutokana na ukosefu wa elimu ya kutosha kwa
wananchi juu ya ugonjwa huu, baadhi yao wamekuwa wakihusisha matukio ya
vifo hivyo na imani ya kishirikina,” alisema Kebwe na kuongeza: “Mtu
akifa watu wanasema kalogwa, mara kuna mkono wa mtu, kumbe kifo hicho
kimetokana na ugonjwa wa ‘Sickle Cell’. Tuachane na imani hizo potofu
twende hospitali tukapime ili tuweze kuzuia maambukizi.”
Aliongeza: “Ugonjwa huu ni wa kurithi, kama baba
na mama wana vinasaba hivyo, mtoto akizaliwa naye atakuwa na ugonjwa
huu. Nchi za wenzetu wamefanikiwa kupambana nao kwa njia ya kupima,
kwani ukipima unajitambua.”
Mkurugenzi wa Asasi ya Motion Art Production
(MAP), Honeymoon Aljabry alisema ugonjwa huo umesambaa kwa kasi nchini
na kuiomba Serikali kufanya jitihada za dhati kuokoa maisha ya watu.
Asasi ya MAP kwa kushirikiana na Taasisi ya Fight
Sickle Cell out of Afrika ya nchini Marekani ndiyo walioandaa kampeni
hiyo inayosaidia vifaa vya tiba kwa wagonjwa.
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment