Home » » DODOMA KUPATA LAMI ZAIDI

DODOMA KUPATA LAMI ZAIDI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Dodoma kupata lami zaidiJUMLA ya sh. bilioni 491 zinatumika kujenga barabara ambazo zinazunguka mji wa Dodoma kutokana na mkoa huo kukua kwa kasi.
Hayo yalielezwa na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli hivi karibuni alipokuwa akizindua taa za barabarani mjini Dodoma.
Dk. Magufuli alisema kuwa serikali imewekeza mabilioni ya fedha katika mji wa Dodoma, kwa ajili ya ujenzi wa barabara zinazounganisha mji huo.
“Kwa sababu ukitoka Dodoma kwenda Iringa barabara ya lami inajengwa na inakaribia kumalizika, kutoka Dodoma mjini hadi Mayamaya, Bonga hadi Babati kuna makandarasi wanajenga na kutoka hapa kwenda Central Cordor zimeishamalizika, na kutoka hapa hadi Dar es Salaam zimeishamalizika.
“Pamoja na barabara za mjini kumalizika, tunaendelea kujenga barabara nyingine za kutoka Dodoma mjini kwenda Chuo Kikuu cha Dodoma, na miradi hii yote kwa ujumla wake ina zaidi ya sh bilioni 491,” alieleza.
Mbali na hilo, Dk. Magufuli alisema kuwa Dodoma ni makao makuu ya nchi, hivyo kuna kila sababu ya kuhakikisha inajengwa kwa kiwango ambacho kitakubalika
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa