Home » » MUKOBA:UWIANO WA KIUCHUMI NI MKUBWA

MUKOBA:UWIANO WA KIUCHUMI NI MKUBWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

RAIS wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, amesema pamoja na uchumi kuonekana umekua, bado uwiano kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho ni mkubwa.
Mukoba alitoa kauli hiyo muda mfupi baada ya uzinduzi wa baraza kuu la tatu la wafanyakazi katika utumishi wa umma Tanzania Bara lililofanyika mjini hapa.
Alisema inashangaza kuona kipindi ambacho inasemekana kuwa uchumi wa nchi umekua ndicho kipindi ambacho watumishi wamekuwa wakifanya vibaya zaidi, jambo ambalo linatia shaka na kuonyesha wazi kuwa watumishi bado wana madai ambayo hayatekelezeki.
“Miaka ya 1980 watumishi walikuwa wakitembea mwendo mrefu kufuata mishahara ama kufuata mahitaji kutokana na miundombinu mibovu, lakini miundombinu mizuri, lakini watumishi wanafanya kazi vibaya tofauti na miaka hiyo, hapo inaonyesha kuwa ni kutokana na kutokuwepo kwa mgawanyo wa rasilimali za nchi zilizopo. Lipo kundi dogo ambalo linapata mgawanyo mkubwa wa rasilimali na kundi kubwa linapata rasilimali kidogo za nchi,” alisema.
Awali Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Pindi Chana,  akizungumza kwa niaba ya Waziri wa wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani, alisema hivi sasa wananchi wanazielewa haki zao na wanaweza kudai huduma bora na kuhoji utendaji wa serikali kwa kutumia vyombo mbalimbali vya habari.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa