Home » » SHERIA YA FAINI BIDHAA FEKI KUREKEBISHWA

SHERIA YA FAINI BIDHAA FEKI KUREKEBISHWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini (TFDA) inakusudia kuanza mchakato wa kuifanyia marekebisho sheria yake Septemba mwaka huu, ili kuiwezesha kutoza faini watu watakaopatikana na bidhaa bandia ama zisizokidhi viwango.
Hayo yalisemwa jana na meneja wa Kanda ya Kati wa TFDA, Florent Kyombo, alipokuwa akizungumzia tatizo la vyakula na dawa bandia.
Alisema sheria ya sasa inairuhusu mahakama kutoza faini badala ya mamlaka, jambo ambalo limekuwa likifanya utoaji adhabu kuchukua muda mrefu. “Septemba mwaka huu mamlaka itaanza kupitia upya ili tutoze faini sisi badala ya kwenda kortini,” alisema. (Sharon Sauwa)
Chanzo:Mwnanchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa