Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
VITENDO
vya ujangili vinavyoendelea kushamiri nchini, vimechangia taifa
kukumbwa na hatari ya kutoweka kwa wanyamapori wakiwemo tembo na faru.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa na Profesa Davis Mwamfupe wa Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam, alipokuwa akitoa mada kwenye semina ya
kuwajengea uelewa wabunge katika kulinda wanyamapori, iliyoandaliwa na
Chama cha Wabunge cha Kuhifadhi na Kulinda Wanyamapori.
Profesa Mwamfupe alisema hivi sasa wanyama hao ambao walikuwa wengi
katika mbuga na hifadhi mbalimbali nchini, wamepungua kwa kiasi kikubwa.
Alisema hakuna takwimu zinazoonyesha kuongezeka kwa wanyama hao, bali kupungua kutokana na vitendo vya ujangili.
Alieleza kuwa hali hiyo inatokana na uelewa mdogo wa wananchi kuhusiana na faida za wanyamapori.
“Hali hii ndiyo iliyotupa mwamko wa kutoa elimu kuhusiana na hifadhi
za wanyamapori na thamani ya wanyama hao, lakini pia hali halisi
inayoendelea hivi sasa kuhusiana na wanyamapori,” alisema.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment