Home » » WIZARA YA MIFUGO YABANWA NANENANE DODOMA

WIZARA YA MIFUGO YABANWA NANENANE DODOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WIZARA ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi imetakiwa kuhakikisha inawapa washindi wote zawadi walizoahidi katika kilele cha maonyesho ya Nanenane 2013 kabla ya kuanza kwa maonyesho ya Kanda ya Kati Agosti mosi mwaka huu ili kuondoa ubabaishaji.
Agizo hilo limetolewa mjini hapa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Rehema Nchimbi, wakati wa kikao cha pili cha maandalizi ya maonyesho na mashindano maalumu ya mifugo kitaifa na maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kati.
Alisema kitakuwa kitendo cha aibu kama wataanza mashindano mengine bila kuwakabidhi zawadi zao washindi wa mwaka jana.
Kwa upande wake, wizara hiyo ilisema juhudi zinaendelea ili kutekeleza ahadi hiyo kabla ya kuanza kwa maonyesho ya mwaka huu, licha ya kuwa Dk. Nchimbi aliyakataa majibu hayo na kutaka waeleze kwa uwazi zaidi.
Baada ya Dk. Nchimbi kupingana na majibu hayo, walieleza kuwa wanachosubiri ni fedha za matumizi ya kawaida ya ofisi (OC), ya Julai mwaka huu ambayo bado hazijatoka na mara tu zitakapotoka, watawapa washindi wote zawadi zao.
Katika hatua nyingine, Tanzania Daima ilifanya mahojiano na baadhi ya washindi kwa sharti la kutotajwa majina yao kuhusu jambo hilo, ambao wametishia kuandamana kuhakikisha wanapewa zawadi zao kabla ya washindi wa mwaka huu.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa