Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MAONESHO ya wafanyabiashara kipindi cha Bunge la Maalum la Katiba
yanaendelea kwa kasi mjini hapa na kuwakutanisha wajasiriamali zaidi ya
100 katika viwanja vya Mashujaa.
Akizungumza na wandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa wajasiriamali,
Dokta Haruna Kifimbo, alisema lengo kuu la maonesho hayo ni kutoa fursa
kwao kuuza na kunadi bidhaa zao kwa watu mbalimbali wakiwemo wajumbe wa
Bunge hilo.
“Mpaka sasa tuna wajasiriamali 100, ambao wanaendelea na maonesho
yao kwenye viwanja hivi vya Mashujaa kuanzia Agosti 10 mwaka huu, na
maonesho yataendelea mpaka litakapomalizika Bunge la Katiba, hivyo bado
tunaendelea kupokea wajasiliamari wengine zaidi,” alisema Dk. Kifimbo.
Alisema kuwa maonesho hayo yanajumuisha wauzaji wa bidhaa za tiba
mbadala, bidhaa za majumbani, kazi za mikono kutoka ndani na bidhaa
zingine mbalimbali.
Kifimbo ambaye ni mganga wa tiba mbadala alisema maonesho hayo
yatazinduliwa rasmi Agosti 21, mwaka huu, na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk.
Rehema Nchimbi, na kutoa rai kwa wananchi kushiriki.
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment