Home » » WANAWAKE WAUNDA KAMATI MFUMO WA 50/50

WANAWAKE WAUNDA KAMATI MFUMO WA 50/50

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Wanawake waunda kamati mfumo wa 50/50WABUNGE wanawake nchini, wameazimia kuunda kamati ndogo ya wataalamu itakayowashirikisha wanawake kutoka katika mabunge ya Kenya, Rwanda na Uganda ili kutafuta mfumo sahihi wa uwakilishi wa uwiano wa asilimia 50 kwa 50.

Azimio hilo limefikiwa juzi mjini hapa, katika semina ya siku mbili ya mradi wa kuwajengea uwezo wabunge (LSP), iliyoandaliwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Wazo la kufikia uamuzi huo, lilitolewa na mwanaharakati wa masuala ya jinsia, Prof. Ruth Meena, wakati akichangia mada iliyotolewa na Rais wa Wabunge Wanawake Bunge la Afrika, Bernadeta Mushashu, iliyohusu namna ya kuongeza wanawake kufikia 50:50.
Prof. Meena, alisema kuwa pamoja na suala la usawa wa jinsia kukubaliwa na pande zote za wanawake na wanaume, anaona bado kuna hofu na hivyo kupendekeza iundwe kamati hiyo ili upatikane mfumo sahihi ambao utajulikana mapema uweze kuzoeleka.
Katika mada yake, Mushashu alielezea aina tofauti ya mifumo hiyo ya uwakilishi, faida na changamoto zake, kisha akawataka wanawake wachague mfumo uliyo sahihi.
Alisema mfumo wa kwanza ni kuwa na wabunge wawili wawili kila jimbo, ambako watapigiwa kura na wananchi katika jimbo zima la uchaguzi. Kwamba ukichukulia majimbo ya sasa yalivyo, jumla ya wabunge itakuwa 2 x239=478.
Mfumo wa pili ni wa halmashauri kutambuliwa kuwa jimbo, ambapo kutakuwa na wabunge wawili kila jimbo (halmashauri). Kwa mfumo huo jumla ya wabunge itakuwa halmashauri Tanzania Bara + Zanzibar = 168 +10 (2×178= 356).
“Mfumo wa tatu ni kuendelea kuwa na wabunge wa majimbo. Pia kuwe na wabunge wanawake kwenye ngazi ya Wilaya. Wanawake wa vyama vyote wagombee hiyo nafasi ya kiti cha Wilaya na wapigiwe kura na wakazi wote katika wilaya husika. Hii itafanya jumla ya wabunge wote kufikia, (jimbo + wilaya  Bara + Zanzibar)  239 + 133 + 10 = 382,” alisema Mushashu.
Aliongeza kuwa, pia kuwe na kiti cha mbunge mwanamke kwenye ngazi ya halmashauri ili wanawake wa vyama vyote wagombee hiyo nafasi ya kiti cha halmashauri na wapigiwe kura na wakazi wote katika halmashauri hiyo.
Kwamba hiyo itafanya jumla ya wabunge wote kufikia (jimbo +
halmashauri)= 239 + 168 + 10 = 417.
Naye mbunge wa Viti Maalum, Anna Abdallah aliwatahadharisha wanawake kwamba mfumo huo wa uwiano wa jinsia unaopendekezwa wa asilimia 50/50 hautatumika katika uchaguzi mkuu ujao 2015, ikiwa hawatasimamia suala hilo liingizwe kwenye mabadiliko ya 15 ya katiba ya mwaka 1977 yatakayofanyika
Chanzo:Tanzani Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa