Home » » HOSPITALI MVUMI HAINA MASHUKA

HOSPITALI MVUMI HAINA MASHUKA

HOSPITALI Teule ya Mvumi iliyoko wilayani Chamwino, inakabiliwa na upungufu wa mashuka, magodoro na dawa mbalimbali.

Akizungumza na Tanzania Daima juzi, Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk Makundi Godfrey, alisema magodoro, mashuka na dawa katika hospitali hiyo ni tatizo na kusababisha wagonjwa kupata shida.

Kutokana na tatizo hilo, wakati mwingine wagonjwa wanaolazwa hapo wanalazimika kuja hospitali na mashuka yao.

Pamoja na kuwapo kwa uhaba wa dawa na vitendea kazi, bado wagonjwa wamekuwa wakiongezeka, jambo linaloongeza tatizo kwa wauguzi na waganga.

Kutokana na tatizo hilo, Mbunge wa Mtera, Dk John Malecela, alitoa vyandarua 100 kwa ajili ya wagonjwa na kina mama waliojifungulia hospitalini hapo.

Dk Malecela alisema vyandarua hivyo vinatakiwa kutumika kwa walengwa, badala ya kutumiwa na wafanyakazi wa hospitali hiyo, kwani iwapo vyandarua havitawafikia walengwa ni wazi kampeni ya kutokomeza malaria haitafanikiwa.
 Chanzo;Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa