Marehemu, Mez B akiwa studio enzi za uhai wake.
ALIYEKUWA memba wa kundi la Chamber Squad, Moses Bushagama ‘Mez B’
ambaye amefariki jana mjini Dodoma anatarajiwa kuzikwa Jumatatu katika
makaburi ya Wahanga yaliopo Maili Mbili mjini Hapo. Mtandao huu uliongea
na mama wa marehemu, Marry Mkandawile ambaye alisema kuwa kwa sasa
msiba upo maeneo ya Kisasa mjini hapo.UJUE UNDANI WA MEZ B
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva aliyekuwa akiwika na kundi la Chamber Squad, Moses Bushagama ‘Mez B’ amefariki dunia asubuhi ya leo majira ya saa 4:30 mjini Dodoma.Hii imekuwa ni pigo la pili kwa kundi la Chamber Squad kupoteza memba wake baada ya awali kumpoteza Albert Mangweha ‘Ngwear’.Katika makala haya yanauelezea undani wa Mez B mpaka kufikia umauti.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment