Home » » MKUTANO WA NNE WA WADAU WA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF WAFANA MJINI DODOMA'>MKUTANO WA NNE WA WADAU WA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF WAFANA MJINI DODOMA

MKUTANO WA NNE WA WADAU WA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF WAFANA MJINI DODOMA'>MKUTANO WA NNE WA WADAU WA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF WAFANA MJINI DODOMA

Waziri Mkuu,Mizengo Pinda (Kushoto) akizindua huduma mpya itolewayo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF, ya Fao la Uzazi, mwanzoni mwa mkutano mkuu wa wadau na wanachama wa Mfuko huo mjini Dodoma jana. Wanaoshuhudia kutoka kulia, ni naibu waziri wa fedha, Adam Malima, Mwenyekiti wa bodi ya Mfuko huo, GHeorge Yambesi, Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Adam Mayingu, na mkuu wa mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa.
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa Nne wa Wadau na Wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ulioanza leo mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ,Adam Mayingu kihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa Nne wa Wadau na Wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ulioanza leo mjini Dodoma.
Waziri mkuu Mizengo Pinda (Kushoto) akipeana mkono na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Adam Mayingu, huku Mwenyekiti wa bodi ya Mfuko huo, George Yambesi, (Kulia), na Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa wakishuhudia, wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa 4 wa wanachama na wadau wa Mfuko huo mjini Dodoma, Jumatano Feb 18, 2015.
Waziri mkuu Mizengo Pinda, akimpongeza Zainab Khalid, mmoja kati ya wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, aliyefaidika na mkopo wa elimu ambapo sasa anasoma chuo kikuu Huria jijini Dar es Salaam. Tukio hilo lilikuwa sehemu ya ufunghuzi wa mkutano mkuu wan ne wa wadau na wanachama wa Mfuko huo mjini Dodoma Jumatano Februari 18, 2015.
Baadhi ya wajumbe wa bodi ya Mfuko wa Pensheni wa PSPF, waliopita na wa sasa, wakipiga makofi wakati waziri mkuu Mizengo Pinda, wakati akifungua mkutano mkuu wa Nne wa wadau na wanachama wa Mfuko huo mjini Dodoma, Jumatano Februari 18, 2015.
Baadhi wa washiriki wa mkutano mkuu wan ne wa wanachama na wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, mjini Dodoma Jumatano Feb 18, 2015.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa