Home » » SHULE YA SEKONDARI MPWAPWA YAFUNGWA KUTOKANA NA UKOSEFU WA CHAKULA

SHULE YA SEKONDARI MPWAPWA YAFUNGWA KUTOKANA NA UKOSEFU WA CHAKULA


Mkoani Dodoma Shule ya Sekondari Mpwapwa iliyopo katika Wilaya ya Mpwapwa ilitakiwa kufunguliwa tangu Aprili 8, lakini imeshindikana kutokana na ukosefu wa chakula.
Akizungumza na MTANZANIA, mkuu wa shule hiyo, Nelson Mbilinyi, alisema walifunga shule kwa ajili ya likizo fupi, lakini hadi sasa hawajajua ni lini watafungua kutokana na tatizo hilo.
“Hadi sasa hatujajua tutafungua lini, lakini leo tuliambiwa kutakuwa na kikao na Ofisa Elimu wa Mkoa (REO) ndipo tutapata uhakika lini tutafungua shule,” alisema.
Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Msalato iliyopo katika Manispaa ya Dodoma, Mwasi Chibuni, alisema licha ya wanafunzi kuendelea na masomo, hali ya chakula si nzuri.
Alisema shule yao haijafungwa, lakini wanaendelea kuona chakula kitaishia wapi ndipo wachukue uamuzi.
“Sisi hatujafunga, tunaendelea hivyo hivyo tunajikongoja ila kama tukishindwa tutafunga,” alisema.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Chiku Galawa, alipoulizwa kuhusu tatizo hilo la ukosefu wa chakula shuleni, alisema hana taarifa vizuri na kwamba atalisemea suala hilo leo atakapowasiliana na maofisa elimu kutoka wilaya zote.


CHANZO GAZETI LA MTANZANIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa