Home » » SPIKA MAKINDA AITAKA SERIKALI KUKETI NA KUTOA TAMKO JUU YA KUWEPO KURA YA MAONI.

SPIKA MAKINDA AITAKA SERIKALI KUKETI NA KUTOA TAMKO JUU YA KUWEPO KURA YA MAONI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkutano wa kumi na tisa wa Bunge la Jamhuri ya Muungano umemalizika usiku  wa manane huku Spika wa Bunge akiigiza Serikali na kamati ya bunge ya masuala ya sheria kuketi baada ya mapumziko ya sikukuu ya Pasaka na kutoa tamko kuhusiana na kuwepo au la kura ya maoni ya katiba pendekezwa na mwenendo wa uandikishaji wapiga kura katika mfumo mpya wa BVR.
Spika amesema ni vyema masuala hayo yakajulikana ili utata ambao unaendelea kulikabili Taifa kuhusiana na uwepo au la kwa kura hiyo ya maoni ya katiba pendekezwa ukamalizika na kuwafanya wananchi wakaweza kuendelea na mambo mengine. 
 
Katika hitimisho la mkutano huo waziri mkuu Mizengo Pinda amelieleza bunge kuhusiana na mustakabali wa muswada wa sheria ya kutambua maamuzi mahakama ya kadhi ambapo amesema Serikali imeamua kulirejesha suala hilo kwa wadau ili utata unaoendelea kuhusiana na muswada huo ukamalizika.
 
Bunge limeahirishwa mpaka tarehe 12 mwezi wa tano ambapo mkutano wa kumi na tisa ambao utakuwa ni wa bunge la bajeti  utaanza.
Chanzo:ITV

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa