Wajumbe
wa Bunge Maalum la Katiba wakifuatilia Semina iliyoandaliwa na Mtandao
wa Wanawake na Katiba kwaajili ya Wajumbe wa Bunge Maalum kuhusu masuala
ya Jinsia na Katiba iliyofanyika Agosti, 2014 kwenye Ukumbi wa Bunge wa
Pius Msekwa Mjini Dodoma.
Mtandao wa Wanawake na Katiba Tanzania unaounganisha wanawake
kutoka asasi za kiraia za nyanja mbali mbali za kisiasa, kijamii na kiuchumi,
unatambua jitihada zote zilizofanywa na zinazoendelea kufanywa katika
kuhakikisha kwamba Katiba Mpya ya Tanzania inajengwa katika misingi ya usawa wa
jinsia. Kwa mtazamo wa Mtandao, Katiba Pendekezwa imejengwa katika misingi
inayotambua ulinzi wa utu, heshima na
haki za wanawake na hivyo inahitaji
kuthaminiwa na kulindwa na wahusika mbalimbali, wakiwemo viongozi wa vyama vya
siasa nchini.
Kwa mantiki hiyo ya kuhakikisha kwamba yaliyomo katika
Katiba pendekezwa yanalindwa, Mtandao wa Wanawake na Katiba umekua ukifuatilia
kwa makini mwenendo wa viongozi, na haswa viongozi wa vyama vya kisiasa katika matamko
yao mbalimbali wanayoyatoa, yakiwemo
yale yanayohusu mapendekezo ya
kubadilisha sheria ya uchaguzi.
Kwa mfano, viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa wamekuwa
wakiikumbusha serikali kuzingatia katika mabadiliko ya Sheria mpya ya Uchaguzi,
madai matano yakiwemo: Ushindi wa Mgombea Urais uwe wa kura za asilimia hamsini
na zaidi, Nafasi ya Mgombea Binafsi itambuliwe, Tume Huru ya Uchaguzi iwepo na
uwezekano wa kupinga matokeo ya uraisi mahakamani.
Hata hivyo, matamko haya hayajumuishi kuingizwa kwa msingi
wa usawa wa jinsia katika mabadilko ya Sheria yanayopendekezwa, pamoja na michakato
mingine mbalimbali ya uchaguzi na matokeo yake. Mwenendo huu wa viongozi wa Vyama
vya Siasa unatushangaza na kutuonyesha kuwa viongozi wengi wa kisiasa hawatilii
maanani ajenda ya kuleta usawa wa jinsia katika uongozi wa nchi hii. Kwa maana
hiyo, viongozi hawa wanaashiria kutotambua
mchango, nguvu, nafasi na haki wa mwanamke katika nyanja hii muhimu na hivyo kuduwazaa
demokrasia na maendeleo ya nchi hii kwa ujumla.
Mtandao wa Wanawake na Katiba unawakumbusha na kuwataka
viongozi hawa kutambua kwamba:
·
Wanawake ni Zaidi ya asilimia 51% ya raia wa
Tanzania ambao utawala wa nchi unawahusu.
·
Wengi wa wanachama wao ni wanawake, na hivyo
wana nafasi kubwa ya kushawishi wananchi kutounga mkono itikadi, sera na
mwenendo wa vyama vyao vya kisiasa;wanawake tumechoka kutumika na vyama vya
siasa kama wapiga debe; wahamasishaji wa michangi ya vyama;
·
Wanawake ni idadi kubwa ya wapiga kura pamoja na
watunzaji wakuu wa familia na amani ya nchi hii;
·
Vyama vya kisiasa visivyozingatia usawa wa jinsia
na hivyo kuchochea sera za kibaguzi havina nafasi katika ujenzi wa taifa letu haswa
kufuatia kukomaa kwa harakati za jinsia nchini
Hivyo basi, tunatoa rai kuwataka viongozi wa vyama vya
kisiasa kuhakikisha wanazingatia yaliyomo katika Katiba pendekezwa na kuendelea
kuyatetea huku wakihakikisha kwamba matamshi na sera za kibaguzi
hazitavumuliwa.
# # #
Kama ungependa habari zaidi kuhusu mada hii, tafadhali
wasiliana na TGNP ambao ni mojawapo wa wanachama wa mtandao kupitia +255754784050.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment