Home » » Wananchi watakiwa kudai Risiti kwenye vituo vya Petroli na Dizeli‏

Wananchi watakiwa kudai Risiti kwenye vituo vya Petroli na Dizeli‏



Na. Johary Kachwamba - MAELEZO, DODOMA


Serikali  imewahimiza Wananchi kudai risiti pindi wanunuapo mafuta kwenye vituo vya kuuza Petroli na Dizeli ili kurahisisha ukusanyaji wa Kodi ya Mapato, Aidha kutokuchukua risiti ni kosa kisheria hivyo wote muuzaji na mnunuzi  wanastahili adhabu kwa mujibu wa sheria.


Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mwigulu Nchemba amesema hayo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Rukia Ahmad, Mbunge wa Viti Maalum aliyehoji kwanini Serikali isitoze kodi kwa jumla pale vituo hivyo vinaponunua mafuta

Mhe. Nchemba amesema ulipaji wa kodi ya mapato hususani kwa makampuni yanayouza mafuta unafuata mfumo wa wafanyabiashara kujikadiria wenyewe na kulipa kodi kama ilivyoainishwa kwenye Sheria ya Kodi ya Mapato sura 132, kisha ukaguzi wa hesabu kufuata baadaye.


“baada ya kubaini kuwa kuna udhaifu katika utoaji risiti ambao husababisha upotevu wa mapato, Serikali imeanzisha mfumo wa matumiz ya mashine ya kodi ya kielektroniki kwenye biashara mbalimbali ikiwa ni pamoja na vituo vya kuuza mafuta” Mhe. Nchemba
Hata hivyo mfumo wa matumizi ya mashine za kodi za kielektroniki katika kutoa risiti za mauzo umetekelezwa kwa awamu mbili, awamu ya kwanza iiwahusu wafanyabiashara waliosajiliwa na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) wakati awamu ya pili inahusu wafanyabiashara wengine waliobaki


“vituo vingi vya mafuta nchini havijasajiliwa na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwa kuwa mafuta ya Petroli na Dizeli hayatozwi kodi ya VAT” aliongezea Mhe. Nchemba


Kodi za Ushuru wa bidhaa, ushuru wa mafuta na ushuru wa Petroli hukusanywa Forodhani mara tu bidhaa hizi zinapoingizwa nchini, isipokuwa kwa mafuta ya Petroli na Dizeli yanayoenda nchi za jirani. Kodi hizi ulipwa forodhani na makampuni yanayoagiza mafuta ya Petrol na dizeli kwa kuzingatia kiasi cha ujazo wa lita zilizoingizwa nchini kabla ya kuuza kwenye vituo vya mafuta.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa