Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na: Immaculate
Makilika na Lydia Churi - MAELEZO, DODOMA.
Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa
Felipe Nyusi amelihutubia Bunge
la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mapema leo mjini Dodoma, ambapo anakuwa ni Rais wa
kwanza wa nchi hiyo kulihutubia Bunge la
Tanzania.
Rais Nyusi alisema ameamua
kufanya ziara hii ya kwanza nchini na kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania kabla ya kulihutubia Bunge lingine lolote la nchi nyingine kutokana
na uhusianao mwema ulipo baina ya nchi
yake na Tanzania. “Nina furaha sana kwa uhusiano mwema wa nchi ya Tanzania na Msumbiji ”, alisema Rais huyo.
Akimnukuu Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Nyerere Rais Nyusi alisema, “Msumbiji ni jirani na ni nchi ndogo hivyo
ni lazima iongeze juhudi ya kupigana hata baada ya Uhuru,
tusisahau kamwe yale tuliyopitia
ili tuwe na Uhuru wa kweli ”.
Aliwataka wabunge wa Tanzania kufanya kazi kwa pamoja ili kuweza kupambana na adui umaskini,
na kuongeza kuwa ameitembelea Tanzania kuona
jinsi ambavyo wanafanyakazi ya uzalendo kwa nchi yao.
Alitoa wito kwa wabunge wa Tanzania kuchangia katika kuimarisha
Uhusiano baina ya nchi hizi mbili na kuhakikisha wanapiga vita ufisadi na
ugaidi ili kuleta maendeleo na kujenga
Amani kwa ukanda huu na Afrika kwa ujumla.
Aidha, Rais Nyusi kabla ya kuhutubia Bunge akifuatana na ujumbe wake kutoka Msumbiji alitembelea
Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma ambapo alizungumza na mwenyeji
wake Mwenyekiti wa CCM Taifa Mheshimiwa
Dkt. Jakaya Kikwete na viongozi wa CCM Taifa pamoja na viongozi wa Chama cha FRELIMO.
Rais Nyusi alisema anafurahishwa
sana na ushirikiano mzuri ulipo kati ya
nchi hizi mbili tangu enzi za kupigania Uhuru, na kuahidi kuwa mawazo mazuri yaliyotolewa
na viongozi wa mataifa haya mawili tangu uongozi wa
Mwalimu Nyerere hadi Kikwete na Samora
Machel hadi Armando Guebuza yatafanyiwa kazi
ili hatimaye kusaidia kwa manufaa ya nchi hizi mbili.
Naye Rais Kikwete kwa Upande
wake, alimshukuru Rais Nyusi kwa kutembelea Tanzania mara tu baada ya Kuchaguliwa kuwa rais wa nchi hiyo tangu achaguliwe ikiwa ni miezi 4 tu iliyopita.
“Tulikua pamoja FRELIMO
ilipoanzishwa, tulikua pamoja wakati uhuru
wa Msumbiji ulivyotishiwa na mabepari
naahidi kuwa tutaendelea kuwa pamoja wakati wote, alisema
Rais Kikwete.
Rais Nyusi aliapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Januari 16, 2015 mara baaada ya Rais Armando
Guebuza kumaliza muda wake. Rais Nyusi alianza ziara yake ya kikazi jijini Dar
es Salaam Mei 17, na baadae
alitembelea Visiwa vya Zanzibar kabla ya kuhitimisha ziara yake kwa kulihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania jijini Dodoma.
0 comments:
Post a Comment