Home » » MAJALIWA: SIKUTEGEMEA JINA LANGU KUTEULIWA NA MHE. RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI

MAJALIWA: SIKUTEGEMEA JINA LANGU KUTEULIWA NA MHE. RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na Ismail Ngayonga
MAELEZO
Dodoma
19.11.2015
WAZIRI Mkuu mteule wa Serikali ya Awamu ya Tano, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa amesema hakutegemea nafasi ya jina lake kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kshika wadhifa wa nafasi hiyo kubwa katika Serikali.  

Alisema Uteuzi huo ulioidhinishwa na Bunge, umedhihirisha imani ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyonayo kwake iliyomwongoza katika kuliwasilisha jina lake Bungeni.

Akizungumza mara baada ya zoezi la uthibitisho wa uteuzi wa jina lake Bungeni Mjini Dodoma (leo), Mhe. Majaliwa ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa alisema kilichopo mbele yake kwa sasa ni kuwatumia Watanzania pasipo kujali itikadi ya vyama vyao.

Aliongeza kuwa mara baada ya kuanza kazi yake atahakikisha anazunguka katika mikoa mbalimbali nchini ili kujua changamoto mbalimbali zinazowakabili Watanzania na maendeleo yaliyofikiwa katika sehemu mbalimbali.

Aidha Mhe. Majaliwa aliwahakikishia Wabunge ushirikiano wa karibu zaidi katika kupokea ushirikiano ili kuweza kuwaletea maendeleo ya haraka Watanzania. 

Awali akitangaza matokeo ya kura zilizopigwa na Wabunge wa Bunge kwa ajili ya kuidhinisha jina hilo, Msimamizi wa jina hilo ambaye ni Katibu wa Bunge, Thomas Kashilill ah alisema katika uchaguzi huo, Mhe. Majaliwa alipata kura za Ndiyo 258 sawa na asilimia 73.5% ya kura zote.

Aidha Kashilillah alisema kura 91 sawa na asilimia 25% ya kura zote zilisema hapana wakati kura 2 sawa na asilimia 0.06% ya kura zote ziliharibika.

Wakizungumzia uteuzi huo, Wabunge mbalimbali Bunge la Jamhuri ya wamesifu uteuzi waMhe. Kassimu Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa kusema ni kiongozi mwadilifu, mchapakazi na asiye na makundi. 

Wakizungumza kwa wakati tofauti mjini hapa katika mkutano wa Bunge mjini Dodoma, wabunge hao walisema, walisema uteuzi wa Mhe. Majaliwa ni chaguo sahihi katika Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Pombe Magufuli kwa kuzingatia kauli ya hapa kazi tu.
Mbunge wa Ismani (CCM), Mhe. Wiliam Lukuvi alisema uteuzi  huo umekuja katika wakati mwafaka kwa kuzingatia  kuwa Mhe. Majaliwa amepata uzoefu wa kutosha katika katika Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI hivyo anao uelewa wa kutosha kuhusu matatizo mbalimbali ya nchi yetu ikiwemo sekta ya Elimu.
“Mhe. Majaliwa ni Mwalimu na mara zote Walimu ni watu wa kujifunza, amekuwa Naibu Waziri TAMISEMI kwa muda mrefu, amejibu maswali mbalimbali Bungeni yanayoihusu TAMISEMI na pia amezunguka katika maeneo mbalimbaliya nchi na kujinea matatizo ya Watanzania, hivyo ni chaguo sahihi”
Naye Mbunge wa Newala Mjini (CCM), Mhe. George Mkuchika alisema Mhe. Rais amaengalia vizuri kuhusu uteuzi wa Mhe. Majaliwa kwani, Mhe. Majaliwa ni kiongozi mwadilifu, mchapakazi na pia ni mmoja wa Viongozi aliyekuwa na  ushirikiano na uhusiano wa karibu na Wabungewote wa Bunge lililopita, na hivyo ana imani kuwa uteuzi wakeutalisaidia Bunge katika kujenga umoja na mshikamano.
Aidha Mbunge wa Kaliua (CUF), Mhe. MagnalEna Sakaya alisema anamfahamu Mhe. Majaliwa kwa kipindi kirefu kama Kiongozi mchapakazi na aliye tayari kujishusha  na kuwatumikia wananchi wote pindi kujali itikadi za vyama vya siasa.
“Namfahamu vizuri sana Mhe.Majaliwa kuliko mtu yeyote kwani amekuwa Mkuu wa Wilaya ya Urambo kwa kipindi cha miaka 5, ambapo alifanya kazi zake kwa ushirikiano mkubwa zaidi na wananchi, hivyo kuteliwa kwake kuwa  Waziri Mkuu  kutalisaidia Bunge na Serikali.”
Mhe. Sakaya alisema , anaunga mkono uteuzi wa Mhe. Majaliwa kwani ni kiongozi asiye na chembe ya ufisadi na iwapo Serikali ingewasilisha jina la Kiongozi mwenye kashfa, wabunge wa kambi ya upinzani wangeungana pamoja kupinga uteuzi wa kiongozi huyo.
Mbunge wa Msalala (CCM),Mhe. Ezekiel Maige alisema Mhe. Rais Joseph Magufuli amemteua mtu sahihi katika nafasi ya Waziri Mkuu, kwani kwa uzoefu alionao ikiwemo nafasi ya Naibu Waziri wa TAMISEMI na Mkuuwa Wilaya utaweza kumsaidia kusimamia shughuli mbalimbali za Serikali ndani ya Bunge.

Mhe.Maige alisema Mhe. Majaliwa ni miongoni mwa Viongozi walio mstari wa mbele katika ulinzi na uhifadhi wa rasilimali za Taifa ikiwemo mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira “kuna wakati Fulani wakati ule akiwa Mkuuwa Wilaya alikoswakoswa msituni  kutekwa na majangili wakati alipoongoza operesheni  ya kuzuia majangili, hivyo ni kiongozi sahihi” alisema Mhe. Maige.

Mbunge wa Momba Mhe. Job Silinde alisema uteuzi wa Mhe. Majaliwa ni chaguo sahihi, kwani ni mtu aliye tayari kujishusha  na kuwa karibu na watu wote pasipo na kujali itikadi ya vyama vya siasa, na hivyo Wabunge wote hawana budi kutoa ushirikiano kwake ili aweze kutekeleza vyema majukumu yake.

“Mhe. Majaliwa amekaa TAMISEMI, na Ofisi ile ni Mhimili wa nchi, hivyo amepata uzoefu wa kutosha kuhusu nini maana ya Serikali na namna inavyoendesha kazi zake na umri alionao ni umri wa kati na ataweza kuendana na kasi ya Serikali itakayoundwa na Mhe. Rais John Pombe Magufuli.” Alisema Mhe. Silinde.

Mhe. Silinde alisema wakati akiwa TAMISEMI, Mhe. Majaliwa alikuwa Naibu Waziri na kuwa chini ya Viongozi wake, Waziri Mkuu mstaafu Mhe. Mizengo Pinda na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Hawa Ghasia, hivyo kupitia Viongozi hao amejifunza masuala mbalimbali ya Serikali ikiwemo usimamizi wa shughuli za Serikali Bungeni.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa