Home » » MWIGULU; WEZIA WOTE WA FEDHA ZA WAKULIMA WAPANDISHWE KIZIMBANI.

MWIGULU; WEZIA WOTE WA FEDHA ZA WAKULIMA WAPANDISHWE KIZIMBANI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba, amewaagiza viongozi kuhakikisha wale wote waliohusika na wizi wa fedha za wakulima kufikishwa mahakamani mara moja.
 
Alitoa agizo hilo bungeni jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, aliyehoji kuhusiana na ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2013 iliyoelezea upotevu wa Sh. bilioni 28 za wakulima wa zao la tumbaku mkoani Tabora.
 
Nchemba alisema hiyo ripoti anaifahamu na kuagiza wale wote waliohusika katika kuwaibia wakulima hao kuchukuliwa hatua.
 
Alisema suala hilo halipo kwenye tumbaku tu, kwani kuna maeneo mengine ambayo yana changamoto hiyo ya wakulima kuibiwa fedha zao na kuahidi kuwashughulikia wote waliohusika baada ya Bunge kumalizika.
 
Alisema serikali imepanga kupitia makato yote yanayokatwa kwa wakulima na ndani ya siku mbili atatoa tamko juu ya suala hilo.
 
Nchemba alisema Rais John Magufuli ameshaonyesha kukerwa na tozo nyingi za makato kwa wakulima, hali ambayo inawafanya wakose maendeleo, hivyo atalishughulikia suala hilo kwa wakati.
SOURCE: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa