Home » » SERIKALI YAANZA KUREJESHA MAWASILIANO KILOMBERO, ULANGA

SERIKALI YAANZA KUREJESHA MAWASILIANO KILOMBERO, ULANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama
Serikali imeanza kurejesha kwa haraka mawasiliano ya barabara yaliyokatika kati ya wilaya za Kilombero na Ulanga, mkoani Morogoro kutokana na mvua zilizonyesha na kusababisha kivuko cha mto Kilombero kuzama.
Akizungumza wakati akitoa taarifa ya awali ya serikali kuhusiana na tukio hilo bungeni jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama (pichani), alisema sasa timu za kazi za kiutendaji zipo kazini kuangalia namna ya kulishirikisha jeshi katika kazi hiyo.
 Alisema serikali ilipata taarifa ya awali juu ya tukio hilo usiku wa kuamkia jana na kwamba kivuko hicho kilikuwa kimebeba abiria  31, magari matatu na bajaj mbili na  mpaka jana kwa taarifa walizokuwa nazo, abiria 30 wameshaokolewa.
Mhagama aliwasihi  wananchi kutulia kwa kuwa serikali tangu ilipopokea taarifa hiyo imekuwa ikishughulikia haraka ili kuona nini kifanyike na kwa wakati gani.

Alitoa wito kwa Watanzania kuchukua tahadhari ya mvua zinazoendelea kunyesha, kwani kwa mujibu wa watabiri wa hali ya hewa, mvua nyingi na upepo mkalai na dhoruba vinatarajiwa kutokea.
 CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa