Home » » VYUO VYA UVUVI KUJENGWA MIKOA YENYE BAHARI.

VYUO VYA UVUVI KUJENGWA MIKOA YENYE BAHARI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha.
Serikali inapanga kujenga vyuo vya uvuvi katika mikoa yote ambayo ina bahari ili kusaidia wananchi kupata ujuzi kuhusiana na shughuli za uvuvi na kujipatia kipato.
 
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha,alisema hayo jana bungeni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mchinga, Hamidu Bobali, aliyetaka kujua kama serikali haioni umuhimu wa kujenga chuo mkoani Lindi ambako kuna Bahari ya Hindi ili kuwaongezea vijana hao ujuzi na kupata ajira.
 
Ole Nasha alisema Rais John Magufuli, ameonyesha nia ya dhati ya kutaka kuwasaidia wananchi na wizara yake inatambua umuhimu wa kuwafundisha vijana mbinu sahihi za kufanya shughuli za uvuvi, kilimo na ufugaji na ndiyo maana kupitia Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi imeanzisha Chuo cha Uvuvi Mikindani kwa lengo la kusogeza huduma ya mafunzo ya uvuvi kwa wananchi wakiwamo vijana walioko ukanda wa kusini mwa Tanzania ikiwemo Lindi.
SOURCE: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa