Home » » WABUNGE WAPANIA 'KUILIPUA' SERIKALI LEO.

WABUNGE WAPANIA 'KUILIPUA' SERIKALI LEO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais Dk. John Magufuli.
Aidha, alisema kutakuwa na shughuli za chaguzi mbalimbali za kuwapata viongozi wa bunge na wawakilishi wa bunge katika vyombo na taasisi mbalimbali.
 
Alifafanua kuwa, leo utafanyika uchaguzi wa wenyeviti watatu wa bunge na kwamba juzi Kamati ya Uongozi ilipendekeza majina ya wabunge watatu ambao ni Najma Giga, Andrew Chenge na Mary Mwanjelwa kuwania uenyekiti huo.
 
Mbali na uchaguzi huo pia kutakuwa na uchaguzi  wa wajumbe saba wa Tume ya Utumishi wa Bunge, wajumbe watano wa Bunge la Afrika (PAP), wajumbe watano wa Jukwaa la Wabunge wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-PF), Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe 12 wa Kamati ya Utendaji wa Bunge la Jumuiya ya Madola (CPA) pamoja na  wajumbe watano wa Umoja wa Mabunge duniani (IPU).
 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Mbunge wa Viti Maalum, Rose Kamili (Chadema), alisema kwa sasa wanaangalia suala la Zanzibar na hatma yake.
 
Naye Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche(Chadema), alisema kabla ya kuanza kujadili mpango wa maendeleo ya taifa, watahakikisha bunge linajadili hali ya kisiasa Zanzibar kwa sababu mpango unajumuisha na Zanzibar na ni kwa Watanzania.
 
Alisema katika kujadili hotuba ya rais na mpango huo, lazima serikali iseme wamefikia wapi kuhusu suala la Escrow kwa watu waliochukua fedha kwa magunia katika benki ya Stanbic ili wajulikane ni akina nani.
 
"Katika mpango wa miaka mitano ambao tumeuona, Janeth Mbene ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, amekiri serikali ilifanya makosa kubinafsisha viwanda, hivyo serikali inatakiwa ikiri kuwa ilifanya makosa kuuza nyumba hizo.
 
"Kwenye mpango huu, wamezungumza kupunguza matumizi ya serikali wakati majaji, makatibu wakuu na wakuu wa idara mbalimbali wanakaa kwenye mahoteli Dar es salaam,"alisema Heche.
 
Alisema lazima serikali ikiri pia katika hilo, na kwamba mpango huo umejaa takwimu za uongo, huku akitolea mfano upatikanaji wa maji ambao alisema mpango uliweka wazi kuwa unasema maji yamepatikana kwa asilimia 68 wakati hata katika jimbo lake hakuna huduma hiyo.
 
"Maji hayapo kule, hizi ni takwimu za uongo za kupika, hakuna kitu kilichofanyika, hizo asilimia 68 wamezitoa wapi? Haya kwenye afya juu ya kupunguza vifo vya akina mama na watoto, sera ya afya inasema kila kata kutakuwa na zahanati na kituo cha afya lakini kwenye jimbo langu lenye kata 26, tatu tu ndio zina vituo vya afya, vijiji vingi havina zahanati, nadhani ni mambo ambayo yataibuka katika kujadili huu mpango,"alisema Heche.
 
Alisema ukizungumzia kipindupindu, ni dalili kuwa bado hakuna maji safi na salama, hivyo mpango kama unasema uongo haiwezekani kujadili kwenda mbele, lazima useme ukweli kwa takwimu halisi.
 
Naye Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Upendo Pendeza, alisema kwanza watataka serikali iseme ni kwa vipi itashirikisha sekta binafsi katika kuhakikisha uwekezaji wa viwanda unakuwa na tija.
 
"Kwenye hotuba yake rais, alisema mambo ya viwanda, lakini ukiangalia kwenye maeneo mengi wanazungumzia kuacha suala  hilo kwa sekta binafsi, kwa hiyo sisi tunataka aeleze vizuri kwa namna watakavyoshiriki kwenye suala la viwanda na ajira ziongezeke kwa vijana," alisema Pendeza.
 
Mbunge wa Mtera Livingston Lusinde (CCM),  alisema ataibua suala la Bandari Kavu Dodoma.
 
Pia, alisema takwimu ambazo serikali imewasilisha bungeni juu ya maji vijijini kupitia mpango wa maendeleo ya awamu ya pili hazipo sahihi kwa hiyo ataitaka serikali iwasilishe majina ya vijiji vilivyopata maji.

CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa