Home » » MABARAZA YA WATOTO YATATHMINIWA.

MABARAZA YA WATOTO YATATHMINIWA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeanza kufanya tathmini ya utendaji wa mabaraza ya watoto ngazi za kata, wilaya, mkoa na taifa katika mikoa sita ya Tanzania bara.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamis Kingwangala alisema hayo bungeni jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Kibamba, John Mnyika (Chadema) Katika swali lake, Mnyika alitaka kufahamu lini serikali itawasilisha taarifa ya tathimini ya utendaji wa mabaraza ya watoto na walemavu na serikali imefikia hatua gani katika kuwezesha kufanya kazi kwa baraza la vijana la taifa baada ya sheria yake kupitishwa.
Dk Kingwangala alisema tathmini imeanza kufanyika katika mikoa sita nchini, lengo kuu lake ni kubaini hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa malengo ya mabaraza kama ilivyokusudiwa katika uanzishwaji wake.
Alisema hilo litakamilika Mei mwaka huu na mara baada ya kukamilika Wizara itaandaa ripoti ambayo itaonesha matokeo ya tathmini ya utendaji wa mabaraza katika ngazi zote na kuiwasilisha kwa wadau.
Alisema baraza la taifa la ushauuri la watu wenye ulemavu lilizinduliwa Novemba mosi, 2014 lakini kutokana na ufinyu wa bajeti baraza hilo lilifanya kikao chake cha kwanza Januari 14 na 15, 2016.
Alisema serikali itafanya tathimni na kutoa taarifa baada ya kumalizika kipindi cha mwaka mmoja baada ya baraza hilo kuanza kufanya kazi.
CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa