Home » » SERIKALI YAANZA UDHIBITI UUZAJI HOELA TANZANITE.

SERIKALI YAANZA UDHIBITI UUZAJI HOELA TANZANITE.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
SERIKALI imefunga ofisi ya kuuza madini ya tanzanite iliyopo London nchini Uingereza ili kuhakikisha madini hayo yanauzwa nchini tu. Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema hayo jana wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu (CCM) aliyetaka kufahamu mpango wa serikali katika kuhakikisha madini ya tanzanite yanatambulika kama mali ya Tanzania.
Akijibu swali hilo, Waziri Muhongo alisema serikali itahakikisha madini hayo yanauzwa nchini. “Hata London tumefunga ofisi, tunataka madini hayo yauzwe hapa nchini tu,” alisema Profesa Muhongo.
Aidha, Mbunge wa Simanjiro, James Millya (Chadema) akiuliza swali la nyongeza, alitaka kufahamu lini serikali itasaidia vijana waliojiingiza kwenye uchimbaji madini kutokana na kunyanyasika na hatua gani zinatumika kudhibiti soko la madini ya tanzanite.
Akijibu maswali hayo, Profesa Muhongo alisema si kweli kama serikali haijawasaidia wachimbaji wadogo. “Serikali isingewathamini wasingenichagua kuwa mlezi wao kitaifa,” alieleza.
Alisema Serikali imekuwa ikitoa ruzuku kwa vikundi ambapo kila kikundi kilipewa Dola za Marekani 50,000 (Sh milioni 105) na ruzuku ya jumla ni Dola za Marekani 100,000 (Sh milioni 210), na Shirika la Madini la Taifa (STAMIC0) limeweka Idara kwa ajili ya wachimbaji wadogo.
Alisema utafiti umekuwa ukifanyika kabla ya kuwapatia wachimbaji wadogo maeneo. Akijibu maswali ya msingi ya Millya, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani alisema Serikali ya Tanzania inawasaidia wafanyabiashara wa madini wakiwemo wa tanzanite kwa kuwawekea mazingira mazuri ya kibiashara kwa kuhakikisha wanakuwa na leseni halali ili wafanye biashara zao kiuhalali kwa kutumia mitaji yao ya fedha na kulipa kodi stahiki kwa mujibu wa sheria.
 CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa