Home » » SERIKALI YAKABA KOO WAUZA 'UNGA'

SERIKALI YAKABA KOO WAUZA 'UNGA'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
SERIKALI imeongeza juhudi kuhakikisha wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya wanakamatwa na kuadhibiwa vikali kupitia Sheria Namba 5 ya Mwaka 2015.
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana na Ajira, Dk Abdallah Possi alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Mwantumu Dau Haji (CCM). Katika swali lake, mbunge huyo alitaka kufahamu serikali imejipanga vipi kuona inawanusuru vijana katika janga la dawa za kulevya.
Akijibu swali hilo, Dk Possi alisema serikali inatambua kuwa matumizi ya dawa za kulevya yana madhara mengi kwa watumiaji, familia na jamii kwa ujumla. Dk Possi alisema ili kunusuru vijana na madhara hayo, hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kuendeleza huduma njema na endelevu ya serikali ya kutoa matibabu kwa watumiaji wa dawa za kulevya katika hospitali na vituo vya magonjwa ya akili ili kuwasaidia watumiaji wa dawa hizo.
Alisema hatua nyingine zilizochukuliwa ni kuratibu na kusaidia kuanzishwa kwa nyumba za ushauri na upataji nafuu na huduma za kuwafikia watumiaji katika miji mbalimbali nchini. Dk Possi alisema hatua nyingine ni kuanzisha huduma ya tiba kwa kutumia dawa ya methadone kwenye hospitali. Akijibu swali la nyongeza la mbunge huyo, Dk Possi alisema mtu yeyote mwenye taarifa ya askari wanaowalinda watumiaji wa dawa za kulevya waziwasilishe.
CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa