Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais John Magufuli
Chamacha Walimu Tanzania (CWT), kimeanza kuibip
serikali ya Rais John Magufuli kwa kuitaka a iwe imelipa madai yao
kabla maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) mwaka huu
ili kuepusha sherehe hizo kuingia doa.
Rais wa CWT, Gratian Mukoba, alisema jana kuwa uamuzi huo umetokana
na maazimio ya Baraza Kuu la Chama hicho, lililokaa Januari 28 hadi 30
mwaka huu mkoani Dodoma.
Alisema chama hicho kinataka kuona wanachama wake wastaafu
wanalipwa mafao yao haraka na kwamba Baraza Kuu pia limeazimia pia
kuwapeleka walimu wake ambao hawajapanda madaraja kwa wakurugenzi wa
halmashauri ili wawape barua za kupandishwa madaraja.
Mukoba alisema anajua umuhimu wa sherehe za Mei Mosi na asingependa
kuona zinakwama hasa ikizingatiwa kuwa ni sherehe za kwanza kwa Rais
Magufuli, lakini ni lazima wastaafu walipwe mafao yao na walimu
waliokwama kupandishwa madaraja wapandishwe.
“Sheria inasema mtu aliyecheleweshewa mafao anastahili kulipwa
nyogongeza ya asilimia 15 ikiwa ni fidia ya usumbufu, hivyo tunaomba
watakapowalipa wawape na hiyo nyongeza, maana wamewasumbua sana na
wakaurugenzi wa manispaa nao wawape barua za kuwapandisha madaraja
walimu ambao wanasotea barua hizo,” alisema Mukoba.
Mukoba alisema kuna walimu zaidi ya 200 ambao walistaafu, lakini
bado wanazungushwa zungushwa kulipwa mafao yao na walimu wanaostahili
kupandishwa madaraja hawajapewa barua za kwa muda mrefu, jambo
linalowanyima haki.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment