Home » » MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI, DODOMA.

MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI, DODOMA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Waziri wa Nishati na Mdini, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akisalimiana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi mara walipokutana Bungeni mjini Dodoma wakati wa Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madinileo 19 Me, 2016  bungeni hapo.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Profesa Jumanne Maghembe akiwasili viwanja vya Bunge mjini Dodoma kwa ajili ya vikao vya asubuhi katika Bunge hilo leo 19 Mei, 2016.


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (kushoto) akiwa ameongozana na Mbunge mwenzie wakiwasili viwanja vya Bunge mjini Dodoma kwa ajili ya vikao vya asubuhi katika Bunge hilo leo 19 Mei, 2016.

Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akiwasili viwanja vya Bunge mjini Dodoma kwa ajili ya vikao vya asubuhi katika Bunge hilo leo 19 Mei, 2016.

Naibu Waziri, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhe. William Tate Ole Nasha (kushoto) akiteta jambo na Mbunge wa CHADEMA, Mhe. Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay wakati walipowasili viwanja vya Bunge mjini Dodoma kwa ajili ya Vikao vya asubuhi vya bunge hilo leo 19 Mei, 2016.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba (kushoto) akiwa na Mbunge mwenzie wakiingia ndani ya bunge mjini Dodoma kuhudhuria vikao vya asubuhi vya bunge hilo leo 19 Mei, 2016.


Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe.Angelina Mabula akiwasili viwanja vya Bunge mjini Dodoma kwa ajili ya vikao vya asubuhi katika Bunge hilo leo 19 Mei, 2016.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa akijibu maswali ya papo kwa papo leo Bungeni mjini Dodoma 19 Mei, 2016.



Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Andrew Chenge (kushoto) akiwa ameongozana na Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA, Mhe. Cecilia Paresso wakielekea ndani ya Bunge kwa ajili ya Vikao vya asubuhi vya bunge hilo 19 Mei, 2016 mjini Dodoma.

Baadhi ya Wabunge wa Majimbo mbalimbali wakiwasili katika viwanja vya bunge kuhudhiria vikao vya asubuhi ndani ya bunge hilo mjini Dodoma leo 19 Mei, 2016.

 

Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (mwene gauni la kitenge) akiwa na baadhi ya Wabunge wakielekea ndani ya bunge kwa ajili ya vikao vya asubuhi vya bunge hilo 19 Mei, 2016 mjini Dodoma.



Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akielekea ndani ya bunge kwa ajili ya vikao vya asubuhi vya bunge hilo 19 Mei, 2016 mjini Dodoma.
(Picha zote na Benedict Liwenga, MAELEZO, Dodoma)

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa