Home » » Mbunge atoa tuhuma nzito kwa TRA, TCRA, EWURA

Mbunge atoa tuhuma nzito kwa TRA, TCRA, EWURA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MBUNGE wa Ulanga, Godluck Mlinga (CCM)
MBUNGE wa Ulanga, Godluck Mlinga (CCM) ameyatuhumu mashirika ya umma ambayo hayajajiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kuwa watendaji wake wakuu wamepewa malipo ya asilimia 10 ili mashirika hayo kujiunga na kampuni binafsi za bima.

Ameyataja baadhi ya mashirika hayo ya umma yaliyokaidi kujiunga na NHIF licha ya kulazimishwa kisheria kuwa ni Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

“Yapo mashirika ya umma yanakataa kujiunga na NHIF wakati sisi wabunge tumejiunga, wao ni nani? Wakubwa wao wanapata asilimia 10 na wanajiunga na kampuni za bima ya afya binafsi…

“Mimi niliwahi kuwa Compliance Officer wa NHIF nikaenda TRA, nikawaeleza umuhimu wa kujiunga NHIF unachangia pesa kidogo unapata huduma nyingi lakini bosi wao akanijibu pesa si tatizo na afadhali ametumbuliwa huyo bosi wao, yule angekuwa ofisini kwangu asingetoka,” alisema Mlinga na kuongeza:

“Kila sehemu wananitaja Mlinga Mlinga, napata vitisho vingi lakini serikali inanilinda na kama jeshi (JWTZ) limeweza kusambaratisha M23 itashindwa kunilinda mimi…wengine wananiita teja hivi teja anavaa suti iliyonyooka kama mimi, siwezi kukasirika kwa sababu si kweli lakini wangeniita mbilikimo ningekasirika kwa sababu kweli.”

Mbunge huyo alitaka serikali ikomeshe tabia ya wanaume kubaka wazee na kufafanua “najiuliza wanawake wa mikoa yenye ubakaji wa wazee ni wagumu kuelewa hadi wazee wabakwe?”

Naye Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby (CCM) amesema sasa ataanza kuacha kuwashawishi wananchi wake kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) kutokana na mfuko huo kutopeleka dawa na chanjo za watoto kwenye vituo vya afya, badala yake inapeleka kondomu na vifaa visivyo muhimu kwa wananchi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa