Na Godfriend Mbuya
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Jonathan
Lema (Chadema) amesema kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. John Magufuli alichelewa kumng'oa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Charles Kitwanga katika wadhifa wake.
Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya
Ndani ya nchi ameyasema hayo katika mahojiano maalum na EATV kuhusu
maamuzi ya Rais kumng'oa Waziri Kitwanga katika wadhifa wake ambapo Lema
amebainisha wazi kwamba Rais alipaswa kutengua uteuzi wa waziri huyo
baada ya kuandamwa na kashfa ya ufisadi kwa kampuni ambayo ana ubia nayo
ambayo ilipewa kazi ya kufanya manunuzi na kuweka mashine za kuhifadhi
alama za vidole katika vituo vya polisi nchini.
''Bunge lilipuuzia maoni ya kambi rasmi ya
upinzani kuhusu suala la Waziri Kitwanga kuhusika katika kampuni
iliyopewa kazi ya kuweka mashine katika vituo vya polisi, kama Rais
alikuwa na nia njema angemsimamisha mapema kupisha uchunguzi, hii ya
kuja kumsimamisha kwa maadili ya unywaji pombe ni issue ndogo
ukilingnisha kashfa ya lugumi''-Amesema Lema.
Aidha Mbunge huyo ameeleza kuwa wakati wa
Bunge la katiba pombe ilikuwa inauzwa bungeni hivyo kitwanga
kusimamishwa kachukuliwa kama sample tuu kwakuwa wabunge na mawaziri
wanaokunywa pombe wakati wa kazi ni wengi zaidi.
0 comments:
Post a Comment