Home » » Serikali kufufua mashamba yote ya kilimo, mifugo

Serikali kufufua mashamba yote ya kilimo, mifugo

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba

SERIKALI imeamua kufufua mashamba yote ya kilimo na mifugo nchini.
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mwigulu Nchemba amesema kwa kuanzia, wiki ijayo maofisa wa Benki ya Kilimo Tanzania watatembelea shamba la mifugo la Kitulo, Makete.
Hatua hiyo inatokana baada ya kuonana na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Daud Yassin aliyekumbushia ahadi ya kufufua shamba hilo.
Mwigulu alisema hayo bungeni wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kasulu Mjini, Daniel Nsanzugwanko (CCM) aliyehoji sababu za kituo cha kuzalisha mbegu cha Bugaga kutelekezwa.
Kwa mujibu wa Mwigulu, serikali itafufua mashamba yote na imekuwa katika maandalizi tofauti kuhakikisha mashamba hayo yanafufuka.
“Nia ya serikali ni kuhakikisha kuwa mashamba yote ya mifugo na kilimo yanafufuka. Tunafanya maandalizi kwa kila eneo husika. Tutahakikisha tunafanya utaratibu wa kuyafufua ili kusaidia vijana katika kilimo na masoko,” alieleza Mwigulu.
Katika majibu yake kuhusu shamba la mbegu la Bugaga, Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha alisema limekaa kwa muda mrefu bila ya kuzalisha kutokana na ufinyu wa fedha, limepangwa kufufuliwa katika mwaka 2016/17 lizalishe mbegu kwa wingi.
Hivi karibuni, Waziri Mwigulu alikutana na Mkuu wa Wilaya ya Makete aliyefika mjini hapa kuonana naye ili kukumbushia ahadi yake ya Machi mwaka huu alipotembelea shamba la Kitulo na kuahidi serikali italifufua shamba hilo.
Chanzo Kutoka Habari Leo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa