Na Benedict Liwenga, MAELEZO, Dodoma.
Serikali
imewaunga mkono Wachimbaji Wadogo wa Madini wa Busiri kwa kuwatafutia
maeneo ya uchimbaji wa madini, ambapo Wizara ya Nishati na Madini
imetenga eneo lenye ukubwa wa hekta 11,031 lililokuwa chini ya Leseni za
Utafutaji namba PL 3220/2005 ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Bw. Daudi
Mbaga pamoja na PL 5853/2009 iliyokuwa ikimilikiwa na na Meru Minerals
Resources Limited ambazo zilizoisha muda wake.
Hayo
yamesemwa leo Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri, Wizara ya Nishati
na Madini, Mhe. Medard Kalemani wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo
la Biharamulo Magharibi kuhusu mikakati ya Serikali ya kuwaunga mkono
Wachimbaji wadogo wadogo wa Busiri.
Mhe.
Kalemani ameeleza kuwa, hadi mwishoni mwa mwezi Machi, 2016, Wizara
yake imegawa kwa wananchi wa Busiri leseni 81 za Uchimbaji Mdogo wa
Madini (PMLs) katika eneo hilo, sawa na takribani hekta 810 kati ya
hekta 11,031 za eneo lililoachwa kwa ajili ya Wachimbaji Wadogo.
“Wizara
imegawa leseni nyingine 30 za uchimbaji mdogo (PMLs) katika eneo
lililopo katika kijiji cha Kuntakama takribani kilomita moja eneo la
uchimbaji mdogo wa madini la Busiri”, alisema, Mhe. Kalemani.
Ameongeza
kuwa, mkakati mwingine wa Serikali ni kuendelea kulitumia Shirika la
Madini la Taifa (STAMICO) kutoa huduma ya ugani kwa wachimbaji madini
wadogo wa kijiji cha Busiri na wengine wote nchini ikiwemo kutoa ruzuku
kupitia Mfuko wa Wachimbaji Wadogo.
“STAMICO
pia itaendelea kuwapa elimu wachimbaji wadogo na kuwahamasisha kuunda
Vikundi vya Uchimbaji ili waweze kusaidiwa kwa pamoja”, alisema Mhe.
Kalemani.
Aidha,
Serikali imekuwa ikiwatembelea wachimbaji madini wa eneo tajwa mara kwa
mara kwa kutumia Maafisa na Wataalamu wa Ofisi ya Kanda ya Ziwa
Viktoria Magharibi na Ofisi ya Afisa Madini Mkazi-Bukoba.
Amefafanua
kuwa, tarehe 11 Machi, 2016 Afisa Madini Mkazi wa Bukoba alifika na
kufanya mkutano na kikundi cha Busiri Mining Co-operative Society
Limited chenye Leseni Na. PML 001712WLZ.
“Ili
kutekeleza ombi la sasa la Mheshimiwa Mbunge, Wizara yangu itamtuma
Afisa Madini wa Kanda ili awatembelee tena na kuwaelimisha juu ya fursa
zilizopo za kuendeleza wachimbaji wadogo ili uchimbaji uwe wenye tija na
kutoa ajira na kuondoa umaskini kupitia uchimbaji wa madini”,
aliongeza, Mhe. Kalemani.
0 comments:
Post a Comment