Jonas Kamaleki
Maelezo
Dodoma
Serikali imewapandisha vyeo askari polisi 1,657 wa vyeo vya uongozi mdogo kwa mwaka wa fedha 2014/2015 kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma.
Akijibu
swali la mbunge wa Kojani, Mhe. Hamad Salim Maalim kwa niaba ya Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Naibu waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi ,
Mhe. William Ole Nasha amesema
askari hupanda vyeo kama ilivyo kwa watumishi wengine wa umma na vyeo
hivi huambatana na kuongezeka kwa maslahi yao kulingana na cheo
alichopandishwa.
Ole
Nasha amekiri kuwepo kwa ucheleweshwaji wa ulipaji wa mishahara
inayolingana na vyeo katika jeshi la polisi na kufafanua kuwa yapo
matatizo ya kiufundi yanayojitokeza wakati wa zoezi la kurekebisha
mishahara ambayo husababisha baadhi ya askari kutorekebishiwa mishahara
yao.
Aliongeza kuwa juhudi hufanyika ili kutatua tatizo hilo mara mhusika anapowasilisha malalamiko yake Makao Makuu ya Jeshi hilo.
Naibu
Waziri huyo alisema Kitengo cha Maslahi Polisi Makao Makuu hupokea
malalamiko yao na kuwasiliana na Mamlaka za ulipaji ili kutatua tatizo
husika.
Ole Nasha ametoa wito kwa skari yeyote ambaye amepatwa na tatizo kama hilo awasiliane
na viongozi katika Kamandi yake au Makao Makuu ya Polisi Idara ya
Maslahi ili kupata ufumbuzi wa tatizo hili haraka iwezekavyo.
Kuhusu
suala la ucheleweshwaji mishahara kuchangia katika vitendo vya polisi
kujihusisha na rushwa, Ole Nasha alisema hilo suala halipo kwani polisi
wanafanya kazi kwa kuzingatia maadili ya kazi na kwamba malalamiko ya
ucheleweshwaji yanapotokea hushughulikiwa.
0 comments:
Post a Comment