Na Mwandishi Wetu, Dodoma
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amezitaka benki nchini zipitie upya riba zao ili Watanzania waweze kukopa na kurejesha kwa urahisi.
Alisema riba kubwa zinazotozwa na baadhi ya benki, huduma zisizokidhi
mahitaji na uelewa mdogo wa masuala ya kifedha, ni miongoni mwa
changamoto wanazokabiliana nazo wananchi wanapotaka huduma za kifedha.
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana alipokuwa akifungua mkutano wa
wadau wa Jumuiya ya Benki za Wananchi (COBAT) uliofanyika mjini hapa.
Mkutano huo ulijumuisha wajumbe kutoka mikoa 10 ya Kigoma, Lindi,
Simiyu, Manyara, Katavi, Mbeya, Mwanza, Morogoro, Singida na Dodoma kati
ya mikoa 18 ya Tanzania Bara ambayo bado haina benki za wananchi ila
ipo katika hatua za kuanzisha.
Alisema changamoto nyingine ni kutokuwepo kwa taarifa mbalimbali za
sheria na taratibu ambazo zinakwamisha ufanisi wa kiutendaji kwa baadhi
ya taasisi, hasa zile zinazolenga kuwahudumia watu wa kipato cha chini.
Chanzo Gazeti la Mtanzania
0 comments:
Post a Comment