Home » » Majaliwa azitaka benki kupitia riba

Majaliwa azitaka benki kupitia riba

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amezitaka benki nchini zipitie upya riba zao ili Watanzania waweze kukopa na kurejesha kwa urahisi.
Alisema riba kubwa zinazotozwa na baadhi ya benki, huduma zisizokidhi mahitaji na uelewa mdogo wa masuala ya kifedha, ni miongoni mwa changamoto wanazokabiliana nazo wananchi wanapotaka huduma za kifedha.
Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana alipokuwa akifungua mkutano wa wadau wa Jumuiya ya Benki za Wananchi (COBAT) uliofanyika mjini hapa.
Mkutano huo ulijumuisha wajumbe kutoka mikoa 10 ya Kigoma, Lindi, Simiyu, Manyara, Katavi, Mbeya, Mwanza, Morogoro, Singida na Dodoma kati ya mikoa 18 ya Tanzania Bara ambayo bado haina benki za wananchi ila ipo katika hatua za kuanzisha.
Alisema changamoto nyingine ni kutokuwepo kwa taarifa mbalimbali za sheria na taratibu ambazo zinakwamisha ufanisi wa kiutendaji kwa baadhi ya taasisi, hasa zile zinazolenga kuwahudumia watu wa kipato cha chini.




Chanzo Gazeti la Mtanzania

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa