Na Jonas Kamaleki
MAELEZO
Dodoma
Tanzania ina upungufu wa maafisa ugani 6,266 ambao serikali inahitaji kuajiri kadri ya upatikanaji wa fedha.
Kauli
hiyo imetolewa leo Bungeni Dodoma na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi,
Mhe. Dkt. Charles Tizeba wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum
(CHADEMA), Mkoa wa Kagera lililoulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Viti
Maalum (CCM), Mkoa wa Kagera, Mhe. Oliva Semuguruka aliyetaka kufahamu
mpango wa serikali katika kuwasaidia wakulima waweze kunufaika na kilimo
cha Ndizi, Kahawa, Mahindi na Maharage.
“Mathalani
mwaka 2006 wizara yangu ilibaini kuwa walikuwepo maafisa ugani 3,377,
ukilinganishwa na mahitaji ya maafisa hao 15,022" alisema Dkt. Tizeba.
Aliongeza
kuwa Serikali inajitahidi kusomesha vijana wengi kwenye vyuo vya kilimo
na kuajiri maafisa ugani 5,377 na kufanya jumla ya wataalam kuwa 8,756
kwa sasa ambao wanatoa elimu na kanuni bora za kilimo.
Tizeba
alisema Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya, inaendelea
kueneza matumizi ya vituo vya rasilimali za Kilimo vya Kata ambapo jumla
ya vituo 322 vimejengwa katika Halmashauri 106 kwenye mikoa 20.
“Kati
ya vituo hivyo vituo 224 vimekamilika na vinafanya ya kutoa mafunzo kwa
wakulima na wafugaji, mashamba ya majaribio, kutoa huduma kwa wafugsjio
na matumizi ya zana za kilimo” alisema Dkt. Tizeba.
Aidha
Waziri Tizeba aliongeza kuwa Wizara yake inaandaa na kurusha vipindi
vya redio kuhusu kanuni za kilimo bora kupitia vituo mbalimbali vyas
redio, ambapo kwa mwaka 2015/16 jumla ya vipindi 122 vilirushwa na
vipindi 52 vilirushwa kupitia TBC Taifa na vipindi 70 vilirushwa kupitia
redio jamii.
Akijibu
swali la nyongeza la Mbunge wa Viti MaaluM (CCM), Mhe. Oliver Semguruka
aliyetaka kujua ni lini bei ya kahawa itapanda ili wakulima wasiuze nje
ya nchi, Dkt Tizeba alisema bei ya kahawa itakuwa nzuri ikiondolewa
kodi 26 zilizopo hivi sasa.
0 comments:
Post a Comment