Na Jonas Kamaleki
Maelezo
Dodoma
KAMBI rasmi ya Upinzani Bungeni imemuunga
mkono Rais, Dkt. John Pombe Magufuli katika juhudi zake za kupunguza
matumizi yasiyo ya lazima na kuelekeza fedha hizo katika miradi ya
maendeleo na huduma za jamii kama ujenzi wa miundombinu ya barabara na
reli.
Pongezi
hizo zimetolewa leo mjini Dodoma na Mbunge wa Momba (CHADEMA), David
Silinde wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu bajeti kuu ya Serikali ya mwaka 2016/17.
“Tunamuunga
mkono Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwa kuondoa posho za vikao (Sitting
Allowances) na tunamwomba aondoe posho hizo kwa wabunge nao watumie
mishahara yao ili kuwe na usawa,” alisema Silinde.
Silinde
alisema kuwa Kambi Rasmi ya Upinzani inaunga mkono juhudi za Mhe Rais
Magufuli za kukusanya kodi ambayo inabidi ielekezwe kwenye miradi ya
maendeleo na huduma za kijamii.
“Tunaungana
na Serikali kukata kodi kwenye kiinua mgongo cha wabunge lakini
tunamuomba Mheshimiwa Rais apanue wigo wa kodi hiyo hadi kwa wakuu wa
Mikoa na Wilaya,” alisema Silinde.
Kwa
upande wake, mbunge wa Jimbo la Vunjo (NCCR-Mageuzi), Mhe. James Mbatia
amesema kuwa Kambi Rasmi ya Upinzani inamuomba Mhe. Rais Magufuli
kufuta posho za vikao kwa wabunge haraka ili kuleta usawa kwa watanzania
wote.
0 comments:
Post a Comment