Na: Frank Mvungi - MAELEZO- Dodoma
Vyombo vya Habari nchini Vimetakiwa kuzingatia weledi katika kutimiza majukumu yake ili kusaidia Taifa kufikia maendelo ya kweli na endelevu.
Kauli
hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt.
Harrison Mwakyembe wakati wa mkutano na vyombo vya habari.
Akifafanua Mhe. Mwakyembe
amesema ili Taifa liwe na Maendeleo ni lazima kuwa na Vyombo vya Habari
vinavyozingatia weledi wa taaluma ya uandishi wa habari pamoja na
Sheria na Kanuni zinazosimamia tasnia hiyo.
“Navipongeza
Vyombo vingi vya Habari hapa nchini ambavyo vinafanya kazi nzuri ya
kuelemisha Umma na kuchochea maendeleo ya nchi yetu ila kuna wachache
ambao kwa makusudi wameamua kupotosha Umma” alisisistiza Dkt. Mwakyembe
Hivi
Karibuni gazeti moja lilitoa taarifa zinapotosha Umma kwa kumhusisha
Waziri huyo na maswala ya Ufisadi ambapo alitumia fursa hiyo kuviasa
vyombo vya habari kuepuka kuandika au kusambaza habari ambazo ni za
upotoshaji na hazina maslahi kwa Taifa na hazijafanyiwa uchunguzi wa
kina.
Akitolea
mfano chombo hicho cha habari Mwakyembe amesema kuwa, kimekuwa
kikiripoti taarifa zinazogusa masuaa ya Ulinzi na Usalama pasipo
kuangalia maslahi ya Taifa kwanza hali inayoonyesha kukosekana kwa
uzalendo.
Mwakyembe
aliongeza kuwa tasnia ya habari imekuwa na ni vema sasa waandishi wote
kuzingatia maadili ya taaluma hiyo ili kuepuka kufikishwa katika vyombo
vya sheria kwa kukiuka sheria na kanuni za uandishi wa habari.
Tasnia
ya Habari ni muhimili muhimu katika kuchochea Maendelo ya Taifa lolote
lile kwa kuelimisha kuhamasisha na kuamsha ari ya wananchi kujiletea
maendeleo.
0 comments:
Post a Comment