Kauli hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Maji, Gerson Lwenge, wakati
akizindua Bodi ya saba ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira kwa
Mji wa Dodoma (Duwasa).
Alisema bodi hiyo ina wajibu wa kuhakikisha inaelekeza nguvu zake
kuhakikisha ujio wa Serikali mkoani humu haukwami kwa sababu ya ukosefu
wa maji.
Alisema Duwasa ina kazi kubwa kuhakikisha uamuzi wa Serikali kuhamia
Dodoma haukwamishwi na ukosefu wa maji. Lwenge alisema wakati huu
Serikali inapojipanga kuhamia Dodoma ni vyema mamlaka hiyo ikatatua
changamoto zote zinazoweza kusababisha kukwama kwa Serikali kuhamia
mkoani humu.
Pia aliitaka mamlaka hiyo kudhibiti upotevu wa maji ili watumiaji wa maji hayo wayapate.
"Mnapoongeza kiasi cha uzalishaji wa maji hakikisheni kuwa kinakwenda
sambamba na ubadilishaji wa miundombinu ya kusafirishia maji hayo ili
kusababisha maji yote yanayozalishwa kuwafikia wateja wenu," alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Duwasa, David Pallangyo, alisema
mradi wa kuzalisha majisafi kwenye Bwawa la Farkwa lililopo wilayani
Chemba utakapokamilika mamlaka hiyo itakuwa na uwezo wa kuhudumia watu
milioni moja.
Alisema kwa kiasi cha majisafi kinachozalishwa sasa katika visima vya
Mzakwe, Duwasa ina uwezo wa kuhudumia watu watakaohamia mjini hapa
katika siku za mwanzo.
Alisema kwa sasa Duwasa ina uwezo wa kuzalisha jumla ya mita za ujazo
wa majisafi 61,500 kiasi ambacho kinatosha kuhudumia wakazi wote wa mji
wa Dodoma na zaidi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Duwasa, Balozi mstaafu, Job Lusinde, alisema
changamoto inayoikabili mamlaka hiyo kwa sasa ni kuongeza uzalishaji
katika Bwawa la Farkwa ili iweze kuhudumia idadi kubwa ya watu
watakaohamia mjini hapa.
CHANZO GAZETI LA HABARI LEO
0 comments:
Post a Comment