Home » » Serikali itaendelea kuzingatia matakwa ya Katiba na Sheria katika kugawa eneo la Jamhuri katika ngazi ya Mkoa na maeneo mengine ya Utawala.

Serikali itaendelea kuzingatia matakwa ya Katiba na Sheria katika kugawa eneo la Jamhuri katika ngazi ya Mkoa na maeneo mengine ya Utawala.



Na Beatrice Lyimo- MAELEZO DODOMA

Serikali itaendelea kuzingatia matakwa ya Katiba na Sheria katika kugawa eneo la Jamhuri katika ngazi ya Mkoa na maeneo mengine ya Utawala.

Akijibu swali la Mbunge wa Hai Mhe. Freeman Mbowe lililohusu ongezeko la ukubwa wa Serikali na Watumishi wake na uanzishwaji wa maeneo mapya, Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene amesema kuwa uanzishwaji wa maeneo mapya ya utawala.

Maeneo hayo ni pamoja na Mikoa, Wilaya, Majimbo, Tarafa, Kata, Vijiji, Mitaa na Vitongoji kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya mwaka 1977 ambayo humpa Waziri mweye dhamana ya Serikali za Mitaa madaraka ya kuweka utaratibu wa kugawa maeneo hayo.

Simbachawene alisema kuwa Serikali itaendelea kugawa maeneo ya utawala kwa kuzingatia msingi na uhitaji wa wananchi, Katiba na Sheria zilizopo.

“Kama nia ni kupunguza gharama, tuunganishe maeneo madogo ili viwe sehemu moja kuwiana na maeneo makubwa, Serikali itaendelea kugawa maeneo kwa misingi ya kuzingatia Katiba na Sheria zilizopo” alifafanua Waziri Simbachawene.

Kuhusu ongezeko la watumishi, Naibu Waziri TAMISEMI Suleman Jaffo alisema kuwa idadi ya watumishi iliongezeka kutoka wastani wa watumishi 222,792 hadi wastani wa watumishi 405, 314 kati ya mwaka 2000 hadi 2015.

Ongezeko hilo limesababisha bajeti ya mshahara kuongezeka kutoka wastani wa shilingi bilioni 668.6 hadi trilioni 3.05.

Aidha, Jaffo aliongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2010 hadi 2015 imeongezeka Mikoa mitano kutoka 21 hadi 26, Wilaya 114 hadi 139, Tarafa 521 hadi 558, Halmashauri 233 hadi 185, Kata 3,833 hadi 4,420, Vijiji 10,376 hadi 12,545, Mitaa 1,975 hadi 4,037 na Vitongoji  57,137 hadi 64,677.

Azma ya Serikali katika mgawanyo huo ni kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuzingatia uwezo wa nchi kiuchumi na kuendelea kuzingatia utekelezaji wake.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dodoma Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa