Home »
» TASWIRA MBALIMBALI LEO BUNGENI MJINI DODOMA
TASWIRA MBALIMBALI LEO BUNGENI MJINI DODOMA
|
Baadhi
ya Wabunge wakiingia katika ukumbi wa bunge kuhudhuria kikao cha 2 cha bunge la
kumi na moja la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania
|
|
Mbunge
wa Jimbo la Urambo Mhe.Margaret Sitta akimueleza Jambo Waziri Mkuu wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa leo Mjini Dodoma.
|
|
Naibu
Waziri Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji akijibu swali wakati wa
kikao cha 2 cha bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania ambapo alitoa wito kwa
waajiri nchini kuwasilisha nyaraka za wastaafu kwenye mifuko ya hifadhi ya
jamii miezi mitatu hadi sita kabla ya kustaafu kwa wateja wao ili kukabiliana
na changamoto zinazoweza kujitokeza.
|
|
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) akimsikiliza Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba Leo
Bungeni Mjini Dodoma.
|
|
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Kintinku mkoni Singida wakifuatili vikao vya Bunge leo
Mjini Dodoma |
|
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba
akijibu swali wakati wa kikao cha 2 cha bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ambapo alisema serikali haina mgogoro wowote wa mafuta baina ya
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, wakati wa kikao cha Pili cha Bunge hilo leo Mjini Dodoma
|
|
Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Wazee na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (MB) akimueleza jambo
Mwansheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju leo Mjini Dodoma.
|
|
Mwenyekiti wa Bunge Mhe. Andrew Chenge akiongoza
kikao cha Bunge leo Mjini Dodoma |
|
Mbunge
wa Jimbo la Kaliua Mhe. Magdalena Sakaya akiuliza swali wakati wa Kikao cha
Pili cha Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
PICHA
NA HASSAN SILAYO-MAELEZO
|
0 comments:
Post a Comment