Na Mwandishi Wetu Dodoma
Chama
cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Taasisi ya Twaweza wamesema kuwa
Muswaada wa Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016 ni bora kuliko
Miswada iliyowahi kuwasilishwa nchini.
Haya
yamebainishwa katika maoni yao waliyowasilisha kwenye Kamati ya Bunge
ya Huduma na Maendeleo ya Jamii leo Mjini Dodoma katika juhudi za
kuufanya Muswada huo kuwa bora zaidi na kupelekea kuapa sheria yenye
tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla.
TLS na Twaweza wamebainisha kuwa Muswada huu ni bora zaidi na utasaidia kuwajengea wadau wa habari nchini heshima kwa kutoa huduma bora kupitia vyombo
vya habari kwa kuzingatia taaluma ya Habari waliyonayo hatua ambayo
inautofautisha na muswada uliowasilishwa Bungeni mwaka 2015.
Kwa mujibu wa maoni yalitolewa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) yamesema Muswada huo mzuri zaidi na unaifuta Sheria ya Magazeti ya Mwaka 1976 hatua ambayo wameipongeza Serikali kwani Sheria hiyo iliwahi kuainishwa kuwa miongoni mwa Sheria 40 na kusadikiwa na Tume ya Jaji Francis Nyalali kama Sheria kandamizi.
Kwa
upande wa Taasisi ya Twaweza wao wamesema kuwa Muswada huo utaanzisha
utaratibu ambao utawatambua waandishi wa habari kwa kuanzisha Baraza
Huru la Habari pamoja na Bodi ya Ithibati ya wanahabari amabazo
zitasimamia kanuni na maadili ya wanahabari, kusimamia viwango na
mienendo ya kitaaluma na kuendeleza vigezo bora vya maadili na nidhamu
miongoni mwa wanahabari.
Kwa mantiki hiyo, maoni yaliyowasilishwa kwa Kamati hiyo yanaendana na Muswada ambao unasisitiza kuanzisha
mahusiano na taasisi nyingine za taaluma ya habari ndani na nje ya nchi
ili wadau wa habari waweze kubadilishana mawazo na kuwa na namna bora
ya kuhabarisha umma katika masuala mbalimbali ya kijamii na kiuchumi.
Aidha,
Baraza huru la habari kutakuwa suluhisho katika kusimamia na kusikiliza
malalamiko ambayo yatawasilishwa kwenye baraza hilo kulingana na kanuni
za maadili ya taaluma ya habari hatimaye kuifanya tasnia ya habari
kuheshimika tofauti na hali ilivyokuwa hapo awali.
Uboreshwaji
wa Muswada huo unalenga kuleta Sheria itakayosimamia Tasnia ya Habari
ili iweze kuendana na wakati pamoja na Sheria za kimataifa na namna bora
ya kuwahudumia wananchi.
0 comments:
Post a Comment