Na Daudi Manongi.
UWEPO wa
kifungu kinachopendekeza uanzishwaji wa Baraza Huru la Habari katika Muswada wa
Huduma ya Habari wa mwaka 2016 utasaidia kukuza maadili na viwango vya taaluma
baina ya wanahabari na Kampuni za habari nchini.
Maoni
hayo yametolewa na Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali (TSN) Dk Jim James
Yonazi leo Jijini Dar es Salaam wakati wa mahojiano na mwandishi wa habari hizi
Ameongeza
kuwa chombo hicho ni umuhimu kusimamia maadili ya Taalum ya habari na kufanya
waandishi wa habari hapa nchini wawajibike kwa kazi zao za kila siku za
kuhabarisha umma.
Mhariri
huyo Mtendaji amewahasa wanahabari kuukubali muswada unaopendekezwa kwani ni
kwa maslahi yao wenyewe na utaipa heshima taaluma hii.
“Sheria
hii ni muhimu sana kwa kuwa ukiangalia katika sekta zingine kama
za Uhasibu, Uhandisi ,wakandarasi na wanasheria wanatambuana
kupitia vyombo ambavyo wamejiwekea wakati sekta ya Habari hakuna kitu
kama hicho kinachoweza kuonyesha huyu ni mwanahabari na hata kufahamu idadi yao
nchini ni ngumu hata kuiendeleza katika viwango vya juu uwezekano huo
haupo”alisema Dk Yonazi.
Aidha
amewataka wamiliki na wadau wa tasnia ya Habari kuangalia mapungufu yake na
kuona ni wapi panatakiwa kuboreshwa na kusisitiza ni vema kuwa na sheria hii
kwanza halafu mapungufu yatafanyiwa kazi baadaye.
Kwa
upande mwingine amewataka wandishi kutokuwa waoga wa muswada huu na kutoa maoni
yao kama wafanyavyo katika mambo mengine na kuwataka kwa sasa kuruhusu
utekelezaji wa muswada huu na kuendelea kuusimamia na kuufatilia ili kujua wapi
kuna tatizo na kuliweka wazi ili liweze kurekebishwa.
Aidha
ameongeza kuwa muswada huo unakusudia kuanzisha Bodi ya Ithibati ya wanahabari
ambayo itasaidia katika kuwatambua waandishi wasio wanahabari ambao
wanachafua taaalum ya habari.
0 comments:
Post a Comment